Sunday, January 9, 2011

KANUMBA AMPA MASHARTI JENNIFER

Kanumba akionekana na Jennifer katika moja ya vipande vilivyomo kwenye filamu ya Uncle JJ
cover la sinema ya This is It
Kanumba akiwa na Hanifa Daud 'Jennifer' akiwa ameshika tuzo na zawadi alizopewa katika ofisi za Steps Entertaiment
Moja ya masharti aliyoyatoa Kanumba kwa msanii kinda, Jinnifer, ni kutoshika chini ya nafasi ya 5 kimasomo. Msimamo huo aliutoa Kanumba wakati akiingia makubaliano na wazazi wa staa huyo mtoto pale lilipojadiliwa suala la elimu. Wazazi wengi husita kuwaruhusu watoto wao wenye vipaji kuvionesha mapema wakihofia kuharibu masomo yao.

Ili kuwahakikishia wazazi wa Jennifer kuwa hatoathirika kimasomo pale atakapojiijngiza kwenye filamu, msanii Kanumba alisema kuwa iwapo Jennifer atashuka chini ya nafasi ya tano, atakuwa amepoteza nafasi ya uigizaji. Kitendo hicho kwa maana nyingine, kilikuwa kama kichochoe cha msanii huyo kufanya vizuri darasani, kwani alishika nafasi ya 2 katika mtihani wa muhula wake wa mwisho. Jennifer ni mwanafunzi wa Diamond Primary School, ya Upanga jijini Dar es salaam.

Sinema iliyomtambulisha mtoto huyu ni This Is It iliyotengenezwa na Kanumba Great Films na kufuatiwa na Uncle JJ, zote zikiwa zinafanya vizuri sokoni. Wiki iliyopita, Jennifer alipata tuzo ya msanii bora chipukizi iliyotolewa na tamasha la filamu zanzibar (Ziff) kutokana na uchezaji wake mzuri katika filamu ya This is It.

Kanumba ana stahili kuwa mfano wa kuigwa kwa maproducer wengine wanaochukua watoto wa watu na kuwaingiza kwenye sanaa. Suala la elimu lipewe kipaumbele na liwe moja ya masharti ya kumfanya mtoto kukubalika kuingia kwenye sanaa. kwa staili hii watoto wengi watanufaika bila kuathiri maendeleo yao ya kielimu.

No comments: