Sunday, February 22, 2009

TATIZO LA MIMBA UTOTONI

Little family ... Alfie (shoto), Chantelle na mtoto wao Maisie



Tatizo la mimba za utotoni si la Afrika tu, bali hata Ulaya lipo. Mtoto Alfie Patten, mwenye umri wa miaka 13, alimpa mimba mtoto mwenzie, Chantelle Steadman mwenye umri wa miaka 15 na kuzaa mtoto salama salimini…ishu hii ya aina yake imetokea nchini Uingereza hivi karibuni.

Dogo alimpachika mimba dogo mwenzie katika usiku mmoja tu waliofanya sex kwa mara ya kwanza, tena bila kondom na hawakujua kama wamepeana mimba hadi baada ya wiki 12 kupita. Mama wa msichana alimstukia binti yake baada ya kumuona ananenepa na kitumbo kinamtoka.

Dogo Alfie bado ana akili za kitoto kiasi kwamba hata bei ya nepi haijui, lakini wazazi wa pande zote mbili wako nao pamoja na wanawapa msaada unaohitajika kama watoto, ingawa wazazi nao ni ‘choka mbaya’, wanaishi kwa ‘posho ya serikali’ tu.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la Uingereza, Alfie anakuwa ‘Baba’ mdogo wa pili nchini Uingereza baada ya Sean Stewart ambaye alikuwa baba katika umri wa miaka 12, mwaka 1998, ambaye nae alimapachika mimba jirani yake, Emma Webster, aliyekuwa na umri wa miaka 15… Hii imekaaje jamani?

No comments: