mjengwablog.com inaendelea na
mchakato wa kumpata kiongozi bora kijana kwa mwaka 2011 kutoka kundi la
wabunge. Kinachopimwa ni mchango wao katika jamii na uwezo wao wa
kujenga hoja zenye kutetea maslahi ya taifa ndani na nje ya Bunge.
Ni
wewe utakayeshiriki kuwapima na kuwachuja kwa kura yako. Lengo hasa ni
kuhamasisha vijana kwenye ushiriki wa masuala ya uongozi. Kujenga
Utaifa na Uzalendo na kujenga misingi ya demokrasia na utawala bora.
Washiriki
watachujwa na kubaki sita watakaoungana na sita wengine kutoka kundi
la wabunge vijana wanawake ambao tayari wameshapatikana kwa njia ya
mchakato kama huu kwenye Mjengwablog.com.
Hatua hii ikikamilika tutaingia katika kile kitakachoitwa 'Mjengwablog
Young Leadership Awards'. Hivyo basi, tutampata mbunge bora kijana wa
mwaka 2011. Kigegezo cha kushiriki: Umri wa Mbunge usizidi miaka 40.
Hatua hii ya mchujo inawahusisha washiriki hawa;
1.January Makamba
2.David Kafulila
3. Zitto Kabwe
4. Felix Mkosamali
5. John Mnyika
6. Joseph Sugu Mbilinyi
7. Steven Masele
8. Mohammed Dewji
9. Moses Machali
10. Ezekiel Wenje
11. Hamis Kingwangwalah
12. Livingstone Lusinde
13. Godbless Lema
14. Highness Kiwia
15. David Silinde
16. Mwigulu Nchemba
17. Peter Serukamba
18. Vicent Nyerere
19. Deo Filikunjombe
Utaratibu wa kupiga kura:
Piga kura yako kwenye kisanduku hapo juu kulia. Kompyuta moja kura moja.
Mpiga kura unaweza kubadilisha kura yako lakini huwezi kupiga kura
mbili kwenye kompyuta moja. Matokeo unayona moja kwa moja. 100% hakuna
Kuchakachua.
Matarajio ya baadae:
Mchakato huu ukikamilika , Mjengwablog.com itaratibu mchakato wa kumpata
kiongozi kijana bora kwa mwaka 2011. Ni kutoka nje ya Bunge na
anatotakana na kundi la viongozi vijana wanaokuja kwa kasi na michango
yao kuonekana kwenye jamii. Ni vijana wenye kusimamia na kutetetea
maslahi ya taifa.
Na
mwisho itakuwa mchakato wa kumpata kiongozi bora kijana wa mwaka 2011
kwenye sekta ya uchumi na biashara. Mchakato utafanana na huu. Nao
watatunukiwa tuzo kwenye ’ Mjengwablog Young Leadership Awards 2011’
ambayo itatolewa katika categories totauti kama inavyoonekana hapa. Na
majina ya washiriki yatatokana na kupendekezwa na watembeleaji wa
Mjengwablog na mitandao mingine kama huu wa JF. Tunakaribisha ushauri
na mawazo hata yenye kushutumu.
Naam, ukisikia "Pyeeee! " - Kimeshapulizwa!- Nenda kapige kura yako!
Maggid Mjengwa,
Mratibu
.
Iringa.
http://mjengwa.blogspot.com
No comments:
Post a Comment