Wednesday, December 7, 2011

Serengeti yadhamini mpambano

Pichani kati ni Mkurugenzi wa Mawasiliano kampuni ya SBL.Teddy Mapunda akikabidhi kombe kwa viongozi wa timu ya Bunge na Timu ya Baraza la Wawakilishi.Pichani kulia ni Kapteni wa timu ya Bunge,Mh Amos Makala na kushoto ni Mwenyeki wa timu ya Baraza la Wawakilishi,Mh Hamza Hassani Juma.
Mkurugenzi wa Mawasiliano kampuni ya SBL.Teddy,Mapunda (kulia), akikabidhi vifaa vya michezo kwa baadhi ya viongozi wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar,Mwenyeki wa timu ya Baraza la Wawakilishi,Mh Hamza Hassani Juma,Meneja Msaidizi wa timu,Mh.Ali Nassor Jazira pamoja na Mh.Dau Hamad Maulid.
Mkurugenzi wa Mawasiliano kampuni ya SBL.Teddy,Mapunda akizungumza mbele ya wanahabari mapema leo Makao Makuu ya ofisi hizo zilizopo Oysterbay,jijini Dar,kuhusiana na udhamini wa mechi kati ya Timu ya Wabunge na Timu ya Baraza la Wawakilishi kutoka Zanzibar,itakayofanyika 9 Desemba kwenye Uwanja wa Uhuru,ikiwa ni sehemu mojawapo ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru,aidha Teddy amesema kuwa udhamini wa timu hizo umegharimu kiasi cha zaidi ya milioni 65.
Kapteni wa Timu ya Wabunge,Mh Amos Makala akizungumza ni namna gani wamejipanga kuhusiana na mechi hiyo itakayokuwa ya kusisimua dhidi ya mahasimu wao Timu ya Baraza la Wawakilishi kutoka Zanzibar.
Mwenyekiti wa timu ya Baraza la Wawakilishi nae akifafanua zaidi namna watakavyowakabili wapinzani wao Desemba 9 mwaka huu ndani ya Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano kampuni yaSBL.Teddy,Mapunda (katikati), akizungumzia namna udhamini wao utakavyokuwa kwa timu hizo, wengine kulia na kushoto ni Nahodha wa timu ya Bunge, Mh Amos Makalla na Mwenyekiti wa timu ya Baraza la Wawakilishi, Mh Hamza Hassani Juma.

No comments: