Monday, March 30, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Dar es Salaam Hands up
Baada ya kuwapata mastaa wa Bongo Flava watakao iwakilisha Wilaya ya Ilala (PICHANI JUU) kupitia shindano la kijanja, ‘Dar es Salaam Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu) linaloendeshwa na Gazeti la Ijumaa linalotoka kila siku ya Ijumaa kupitia safu yake ya burudani, ‘ShowBiz’ sasa ni zamu ya Temeke.

Unachotakiwa kufanya wewe msomaji na mpenzi wa mpambano huo ni kutuma ujumbe mfupi (SMS) ukimtaja msanii wa Bongo Flava ambaye unadhani anastahili kuiwakilisha Wilaya ya Temeke katika shindano hilo kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173.

Kumbuka wewe msomaji na mpenzi wa burudani Bongo ndiyo jaji wa mpambano huo ambao tayari umeanza kuvuta hisia wa watu wengi.
**********************************
Jade; Enzi za uhai wake Aliwahi kujiachia na wanaume hawa!
Leo ndani ya ‘Ebwana Dah!’ tunamuangalia mrembo aliyejipatia umaarufu kupitia Shindano la Big Brother lililofanyika nchini Uingereza 2002, Marehemu Jade Goody aliyefariki hivi karibuni kwa ugonjwa wa kansa.

Kwa mujibu wa mtandao unaodili na uhusiano wa kimapenzi wa mastaa wa Ulaya, enzi za uhai wake, Jade aliwahi kujiachia na mastaa wa kiume watatu akiwemo Jack Tweed aliyefunga naye ndoa siku chache kabla ya kifo chake ambaye hivi sasa anaonekana kuchanganyikiwa kwa msiba huo mzito japo alifahamu mkewe atafariki dunia.

Kabla hajakutana na Jack, Jade alianza kujirusha na kijana Jeff Brazier, mwaka 2002 kabla hajadondokea katika penzi la Ryan Amoo mwaka 2005, ambaye baadaye waliachana na kuanzisha uhusiano na Jack. Jade ambaye alifariki dunia Machi 22, mwaka huu akiwa na umri wa miaka 28 ameacha watoto wawili wa kiume.
************************************
Suma Lee: Park Lane limebaki jina tu
Kutoka pande za Tanga msanii, Ismail Sadiq ‘Suma Lee’ ambaye ni mmoja kati ya wasanii wawili waliokuwa wanaunda kundi la ‘Park Lane’ hivi karibuni amechomoka upya na ngoma yenye jina la ‘Ndani ya One Week’ na kutamka kwamba, ule uvumi ulioenea kuwa aliamua kurudi nyumbani kwao Tanga baada ya kushindwa game hauna ukweli wowote, bali alitokomea kwenye mishemishe nyingine za kutafuta maisha.

Mchizi ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita alidondoka ndani ya safu hii akiwa na afya tele na muonekano mpya, alisema kuwa huo ulikuwa ni uvumi tu, sasa amerudi upya kama yeye na kwamba ndoto za kulirudisha kundi lao la Park Lane haipo tena.

“Kundi lina raha yake na matatizo yake, lakini mtu ambaye hafahamu hawezi kujua, hivi sasa hatuna mpango wa kurudi kama kundi, kila mmoja ataendelea kupiga ishu zake kama yeye. Mimi na Cpwaa huwa tunakutana club na kupiga stori za kawaida tu siyo kuhusu kundi, kinachoendelea kwangu ni ujio wa albamu itakayokuwa na jina la ‘Hesabu za mapenzi’ na jumla ya ngoma kumi, baada ya ‘Ndani ya One Week’ nitaachia kazi nyingine yenye jina la ‘UK Dubai’ iliyofanyika kupitia studio za MJ Records.
**************************************
Mnyalu kuendeleza mpambano wa Inspector na Mwana FA
Msanii Mike Mwakatundu a.k.a Mike T au Mnyalu ambaye hivi karibuni aliachana na ukapera kwa kufunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi ameibuka na kuendeleza malumbano yaliyoanzishwa na Inspector Haroun aliyejibu wimbo wa Mwana FA, ‘Bado nipo nipo’, Chile Kasoga anashuka nayo.

Akipiga stori na safu hii, Mike T alisema kwamba, wimbo wake mpya wenye jina la ‘Wala wasielewe’ aliomshirikisha Mwana FA aliyeimba wimbo wa ‘Bado nipo nipo’ unawazungumzia wana ndoa ambao huzisaliti ndoa zao na kutafuta wapenzi wengine wa pembeni.

“Kwa kifupi nataka kuleta changamoto kwa wasanii wengine waliowahi kufanya nyimbo za aina hiyo wakiwemo Mwana FA na Inspector Haroun, sipendi watu wanifikirie vibaya kwa kuwa yote ni sanaa tu na si vinginevyo,” alisema Mnyalu.
***************************
Maunda, Mwasiti kumtoa Bushoke Pasaka
Kutoka katika familia yenye vipaji vya muziki, msanii Maunda Zorro (PICHANI JUU) na Mwasiti Almasi ndiyo wasichana pekee watakaompiga tafu Rutta Maximilian ‘Bushoke’ kutoka Zizzou Entertainment katika uzinduzi wa albamu yake, ‘Dunia njia’ utakaopigwa ndani ya Ukumbi wa Linas Pub uliyopo mjini Bukoba siku ya Sikukuu ya Pasaka.
Akisema na safu hii, Bushoke alitamka kwamba, mbali na mabinti hao, wasanii kama Ngwea, Blue, Steve na wengine kibao wataungana naye katika zoezi hilo la utambulisho wa albamu yake yenye takribani ngoma kumi na moja.
“Shoo ya pili tutaangusha ndani ya Uwanja wa Kaitaba siku itakayofuata, tunategemea kupata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wa Bukoba ukizingatia hiyo itakuwa mara yetu ya kwanza kudondoka pande hizo. Viingilio katika shoo hizo vitakuwa ni shilingi 10, 000 Linas Pub na 5,000 Kaitaba,” alisema Bushoke.
**********************************

Saturday, March 28, 2009

ZIZZOU YADHAMINI MR. HANDSOME




Baadhi ya washiriki wa shindano la kumtafuta kijana mtanashati wa jiji la Dar es salaam (Mr. Dar handsome) wakiwa katika Salon na duka la Zizzou mchana wa leo katika maandalizi yao ya mwisho kwa upande wa mavazi na kujiweka soap soap. Shindano linafanyika usiku huu, New Africa Hotel na Zizzou Fashions ni mdhamini wa shindano hilo.

Friday, March 27, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!

Ali Kiba
Dully Sykes
Dar es Salaam Hands Up
Shindano lako la kijanja zaidi, ‘Dar es Salaam Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu) limeingia kunako hatua nyingine, baada ya wiki iliyopita kuwapata wakali wa Bongo Flava watakaoiwakilisha vyema Wilaya ya Kinondoni, leo tunadondoka na wasanii kutoka pande za Ilala waliyotajwa na wasomaji kuiwakilisha wilaya yao.

Wasanii hao kutoka Wilayani Ilala ni Dully Sykes, Blue, Ali Kibba, Chidi Benz (La Familia), Soggy Dog, Suma G, Zay B na Akili The Brain. Kabla sijaendelea mbele zaidi nakukumbusha kwamba, shindano hili linazihusu Wilaya tatu za Dar es Salaam, Kinondoni, Ilala na Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa burudani hii utatuambia ni ipi ina wasanii wakali.

Baada ya kuwapata wasanii hao kutoka Ilala, sasa tunaelekeza macho yetu pande za Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa mpambano huu unatakiwa utuambie ni msanii gani anastahili kuiwakilisha wilaya hiyo.

Hivi sasa unatakiwa ututumie ujumbe mfupi ukimtaja msanii wa Temeke ambaye unadhani anastahili kuiwakilisha wilaya hiyo kunako shindano hili, si msanii ambaye unamuona hapa pichani. Baada ya kufanya hivyo tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Mwisho wa kupokea kura zenu ni siku ya Jumanne mchana.
*************************************
Blue
Bushoke: Sasa ni zamu ya Bukoba
Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kuifikia Sikukuu kubwa ya Pasaka, msanii Rutta Maximilian Bushoke anatarajia kujirusha na wakazi wa Bukoba, Mkoani Kagera katika kuadhimisha siku hiyo.

Ndani ya ShowBiz msanii huyo ambaye bado ni memba wa kundi la Makole Hexagon lenye maskani yake pande za Dodoma, alisema kwamba baada ya kuzunguka sehemu mbalimbali nchini akiitambulisha albamu yake mpya, ‘Dunia Njia’ sasa ni zamu ya Bukoba.

“Nikiwa na baadhi ya wasanii wengine wa Bongo Flava, kama Ngwea, Blue, Maunda Zorro na wengine kibao tutapiga shoo ya kwanza ndani ya ukumbi wa Linas Club, siku itakayofuata tutajitupa ndani ya Uwanja wa Kaitaba na kuendelea na uzinduzi huo,” alisema Bushoke.

Aidha, mchizi aliweka wazi kwamba, viingilio kunako shoo hiyo vitakuwa ni shilingi elfu kumi (VIP) na elfu tano kawaida, huku uwanjani ikiwa ni shilingi elfu moja kwa kila mtu.
******* **************
Miss EA 2008 kuanzia A-Town
Shindano la kumtafuta mrembo wa Afrika Mashariki (Miss East Africa) ambalo mwaka jana lilimalizika kwa binti kutoka Burundi, Claudia Noyimana kuibuka na ushindi, mwaka huu linaanzia pande za Arusha ambapo litawakutanisha zaidi ya warembo 20.

Akipiga stori na ShowBiz, mratibu wa mpambano huo, Nicodemus Ngogo wa Kampuni ya Tanzania Full Moon Entertainment alisema kwamba tayari zoezi la kuchukua fomu kwa washiriki limeshaanza, linaendelea hadi Aprili 15, mwaka huu kisha warembo ishirini na tano watakaopatikana wataingia kambini kabla ya kukutana kunako jukwaa moja kwa ajili ya kumpata mshindi kutoka pande hizo za Kaskazini.

“Fomu zinaendelea kutolewa katika sehemu mbalimbali Arusha na Dar es Salaam, baada ya hapo warembo wataingia kambini kwa muda wa wiki mbili kabla ya kupambana jukwani ambapo mshindi ataondoka na gari jipya aina ya Toyo Nadia, huku mshindi wa pili na wa tatu wakijipatia pesa taslim ambazo tutazitaja hivi karibuni,” alisema Ngogo. Naye Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, Omari Mawamba alisema kila kitu kuhusu shindano hilo kinaendelea vizuri.
**************************************************

Thursday, March 26, 2009

KUTANA NA MWANDISHI CHIPUKIZI!!!!


Kwenu wapenzi wa fasihi,
Kama ilivyo ada, hapa Mkahawani Soma kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ni siku ya kukutana na mwandishi. Ijumaa hii ya tarehe 27/03/2009 tutakutana ana kwa ana na mwandishi chipukizi Sandra Mushi mwandishi wa The Rhythm of my Rhyme amabacho kinapatikana hapa kwenye duka la vitabu Soma pamoja na hadithi fupi nyingi za kuvutia ambazo amechapishwa kwenye blog yake
www.sandrasden.com na www.sarahsoulfood.wordpress.com hadithi moja imechapishwa kwenye toleo la kwanza la jarida la fasihi Soma.

Tutapata fursa ya kuhojiana naye, kujadili mashairi na hadithi zake, na pia tutasoma baadhi ya hadithi zake na kughani baadhi ya mashairi yake.

************************************************

Dear literati,
Welcome again at Soma Book Café on Friday Evening 27th March/2009 whereby we will meet face to face with a Book Writer Sandra Mushi the author of Rhythm of my Rhyme a newly released anthology that has gained popularity among people of varied social backgrounds. The book is available at Soma Bookshop. Sandra has also authored several short stories available in her blog www.authorsden.com and www.sarahsoulfood.wordpress.com and one of them is serialized on the first issue of Soma literary magazine.

We will chart with Sandra and talk about her writings, plus we shall recite some of her poems and read from some of her stories. You will also be able to get her to autograph your copy of her book.

Welcome and Karibuni Wote!

JE, UMEWAHI KUFANYA ENEMA?- 2

WIKI ILIYOPITA TULIANZA MAKALA HAYA KWA KUANGALIA SUALA LA UFANYAJI WA ENEMA KWA AJILI YA KUSAFISHA TUMBO, ZOEZI AMBALO HUSAIDIA KUONDOA SUMU MWILINI NA HIVYO KUEPUSHA MWILI NA MARADHI, ENDELEA...
UTAJIJUAJE KAMA UTUMBO WAKO NI MCHAFU?

Ni rahisi sana kujitambua kwamba utumbo wako ni mchafu, lakini kwa bahati mbaya watu wengi huwa hawazitambui dalili hizo na wanaozitambua huzipuuzia. Dalili ya kwanza ni harufu mbaya kutoka mdomoni, licha ya kupiga mswaki kila siku. Harufu mbaya unayoisikia mdomoni haitoki mdomoni, bali hutoka tumboni.

Dalili nyingine ni harufu mbaya ‘unapopumua’, wenye matumbo masafi huwezi kusikia pumzi zao zikitoa harufu mbaya. Dalili nyingine ni kukosa kwa choo kwa siku kadhaa. Katika hali ya kawaida, binadamu anatakiwa kupata choo angalau mara moja kwa siku kama siyo mara tatu. Unapokosa choo kwa siku nzima ili hali unakula mara tatu au mbili kwa siku, tena ‘plate’ nzima, ujue una matatizo.

Lakini dalili nyingine na ambayo imefanyiwa utafiti wa kisayansi, inapatikana usoni mwa kila mtu! Uso wa binadamu unaelezea viungo vyote vilivyomo tumboni kama mchoro wa makala haya unavyoonesha. Kila kiungo kilichomo tumboni, unaweza kujua hali yake kwa kuangalia kiungo kinachofanana nacho usoni.

Kuanzia sasa, anza kujiangalia pamoja na afya yako kwa mtizamo mwingine. Jiangalie ndani ya mwili wako kupitia sura yako, utaweza kujijua ulivyo tumboni mwako kwa kuangalia uso wako tu, kwani kila kitu kinachoendelea tumboni, kinaonekana usoni mwako:

Katika mchoro wa kwanza, viungo vyote vya tumboni (kama mchoro wa pili unavyoonesha mfumo wa tumbo) vimeoneshwa usoni. Napenda kuzungumzia zaidi sehemu ya utumbo mkubwa (Large Intestine) ambao ndiyo mada yetu ya leo na ambao ndiyo huweza kusafishwa kwa kutumia Enema.

Mtu ambaye utumbo wake mkubwa umejaa uchafu, utamjua kwa kumuangalia chini ya macho (kama mchoro unavyoonesha), chini ya macho ya watu hawa huwa yamevimba, na kuvimba huko huwa kunamaanisha utumbo wake umejaa choo au ana matatizo ya figo.

Kama tulivyosema hapo awali, kujaa choo katika utumbo mkubwa ndiyo mwanzo wa matatizo mengine ya kiafya, mifumo mingine ya mwili hushindwa kufanya kazi zake vizuri na hivyo kusababisha matatizo kama shinikizo la damu, saratani, kisukari, matatizo ya figo na kibofu cha mkojo, magonjwa ya viungo na maradhi mengine hata usiyoyajua.

Baada ya kuanza na utangulizi huu, nafikiri sasa umeelewa Enema ina umuhimu gani katika afya zetu. Kama kweli tunataka kuishi maisha yaliyo huru dhidi ya maradhi, hatuna budi kuifanya enema. Wiki ijayo tutaelezea ufanyaji wa enema hatua kwa hatua, kwani ni rahisi na kila mtu anapaswa kufanya japo mara moja kwa mwaka ili kuondoa na kujikinga na maradhi.
Itaendelea wiki ijayo..

Tuesday, March 24, 2009

TRUE LOVE!

The girl in the picture is Katie Kirkpatrick, she is 21. Next to her, her fiancé, Nick, 23.
The picture was taken shortly before their wedding ceremony, held on January 11, 2005 in the US .
Katie has terminal cancer and spend hours a day receiving medication. In the picture, Nick is waiting for her on one of the many sessions of quimo to end.
In spite of all the pain, organ failures, and morphine shots, Katie is going along with her wedding and took care
of every detail. The dress had to be adjusted a few times due to her constant weight loss


cid:4.3701829053@web52511.mail.re2.yahoo.com
Katie, in her wheelchair with the oxygen tube , listening a song from her husband and friends
At the reception, katie had to take a few rests.The pain do not let her to be standing up for long periods

Katie died five days after her wedding day. Watching a women so ill and weak getting married and with a smile on her face makes us think..... Happiness is reachable, no matter how long it last. We should stop making our lives complicated.

THE MESSAGE TO LEARN
* Life is short
*Break the rules
*Forgive quickly
*Kiss passionately, love truly
*Laugh constantly
*And never stop smiling
*No matter how strange life is
*Life is not always the party we expected to be, but as long as we are here, we should smile and be grateful.

Monday, March 23, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Bushoke kujiachia Bukoba Pasaka
Akiwa bado anaendelea kupiga kitabu ndani ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo, Mkoani Pwani, msanii Ruta Maxmiliani Bushoke ‘Bushoke’ anatarajia kuendelea na ziara ya utambulisho wa albamu yake, ‘Dunia njia’ pande za Bukoba, siku ya Sikukuu ya Pasaka.

Akipiga stori na safu hii, Bushoke alisema kwamba akiwa Bukoba, Mkoani Kagera ataangusha shoo mbili mfululizo akianzia ndani ya Ukumbi wa Linas Pub siku ya Pasaka ambapo kiingilio kitakuwa ni shilingi 10, 000 (VIP) na 5, 000 kawaida, ikifuatiwa na ndani ya Uwanja wa Kaitaba siku itakayofuata kiingilio kikiwa ni buku moja kwa kila kichwa.

“Katika msafara huo nitakuwa na baadhi ya wasanii ambao nilizunguka nao mwanzo katika uzinduzi wa albamu hiyo, ambao ni Ngwea, Blue, Maunda Zorro na wengine kibao ambao nitawataja hivi karibuni. Watu wa Bukoba na sehemu za jirani wajitokeze kwa wiingi siku hiyo ili tule sikukuu pamoja,” alisema Bushoke.
**********

Hemedi apata dili Mr. HB
Baada ya ‘kuhaso’ huku na kule akitafuta kutoka, msanii Hemedi Suleiman aliyepitia kunako shindano la ‘Tusker Project Fame’ na kuambulia za uso, sasa ameanza kula matunda ya jasho lake nikimaanisha kuwa, ngoma yake mpya ‘Unachotaka ni mapenzi’ imempa dili la kupiga shoo kunako shindano la kumtafuta Mr. Handsome litakalofanyika Machi 28, mwaka huu, Imelda Mtema anajiachia nayo.

Mratibu wa mpambano huo, Methuselah Magese alisema na safu hii kwamba, Hemedi ni miongoni mwa wasanii chache waliopata bahati ya kusimama katika jukwaa la mpambano huo ambao utapigwa katika Hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.

“Katika shindano hilo ambalo litawakutanisha vijana watanashati zaidi ya kumi majaji watakuwa ni Nasreen Kareem, Big Brother 2007, Richard Bezuedenhout na Steven Kanumba,” alisema Magese.
***********

Kikosi kutambulisha 3 na studio yao mpya
Kutoka pande za Kinondoni, Dar es Salaam, kundi la muziki wa Hip Hop lenye jina la Kikosi cha Mizinga linaloongozwa na msanii Kalama Masoud ‘Kalapina’ linatarajia kudondoka ndani ya Ukumbi wa Msasani Club na kutambulisha ngoma zao mpya pamoja na studio yao waliyoipa Kikosi Records, Edna Katabalo anashuka nayo.

Akipiga stori na safu hii, Kalapina alisema kwamba, tukio hilo kubwa litafanyika ndani ya Ukumbi wa Msasani Club, siku ya Pasaka na nyimbo watakazotambulisha ni Pamoja na Pata potea na Hip Hop Agaist Albino.

“Ngoma zote tutakazotambulisha siku hiyo zimetengenezwa ndani ya studio yetu, Kikosi Records, mashabiki wajitokeze kwa wingi ili tuungane katika vita dhidi ya mauaji ya albino ambayo tumeianzisha kupitia sanaa yetu.
**********

Sunday, March 22, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!


Dar es Salaam Hands up
Hatimaye shindano jipya kabisa na la kijanja ‘Dar es Salaam Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu), tayari limeanza na hawa ndio wakali wa muziki wa Bongo Flava waliotajwa kuiwakilisha Wilaya ya Kinondoni kunako mpambano huo kama tulivyowaomba wasomaji wiki iliyopita.

Wasanii hao kutoka pande za Kinondoni ni Jaffarai, Ray C, Prof. Jay, Fid Q, Kalapina (Kikosi cha Mzinga), A.Y, Mr. Nice, Ngwea, Witness na K-Sher. Nakukumbusha tena, shindano hili linazihusu Wilaya tatu za Dar es Salaam, Kinondoni, Ilala na Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa burudani hii utatuambia ni ipi ina wasanii wakali. Baada ya kuwapata wakali kumi kutoka Kinondoni, sasa tunaigeukia Wilaya ya Ilala.

Unachotakiwa kufanya kwa sasa kabla hatujaingia kwenye zoezi kubwa la kuzipigia kura wilaya ni kututajia jina la masanii ambaye unadhani anafanya vyema ndani ya Wilaya ya Ilala kwa kuandika ujumbe mfupi (SMS) ukilitaja jina lake kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Kumbuka kwamba kila wilaya itawakilishwa na wasanii kumi.
***********

Miss Utalii azama mapangoni na madenti

Miss Utalii 2006-2007, Consolata Rushau ambaye pia ni mwalimu wa shule moja ya msingi Mkoani Tanga, ameonesha yuko karibu zaidi na fani hiyo kwa kuwapeleka wanafunzi wake kunako makumbusho ya mapango ya Amboni yaliyopo mkoani humo kila anapopata nafasi, Imelda Mtema alipiga naye stori.

Akisema na ShowBiz alipotembelea ndani ya ofisi zetu zilizopo Sinza, Bamaga, Dar es Salaam hivi karibuni, mrembo huyo alitamka kwamba, japo amebahatika kuwa mwalimu, mambo ya utalii yako kwenye damu yake na ndio maana hupenda kuwapeleka wanafunzi wake ili wafahamu zaidi mambo ya kiutalii.

“Urembo ni sehemu ya maisha yangu, nafikiria kuwa mwanamitindo maarufu, japo kuna fani nyingine nazipenda kama uigizaji wa filamu na nyingine. Bado sijakata tamaa wala sijaridhika na taji nililonalo, naendelea kutafuta nafasi nzuri zaidi katika tasnia ya urembo ili nifikie levo za kina Naomi Campbell,” alisema.

*******
Misosi na Neno la Mungu
Ukiisikiliza ngoma yake mpya, ‘Mungu yuko bize’ unaweza kudhani kwamba, mchizi sasa anaelekea kwenye wokovu ukizingatia kuwa siku hizi pia hupendelea kutoka ‘kipapaa’, yaani kiutu uzima, mashati ya mikono mirefu na tai shingoni kitu ambacho yeye binafsi hajaweka wazi.

Namzungumzia kijana kutoka pande za Tanga, Joseph Rushahu ‘Bwana Misosi’ ambaye baada ya kuisikia kazi hiyo mpya tuliamua kumtafuta ili kujua nini hasa kimemsukuma akaamua kutoka na ngoma hiyo iliyomshirikisha mwana TMK Family, Said Juma ‘Chegge’.

“Mungu yuko bize’ ni sanaa tu, si vinginevyo ila ni kazi ambayo iko pande zote na kwa madhehebu yote haijambagua mtu. Kuna baadhi ya binadamu huwa wanajifanya wako bize zaidi wakati Mungu yuko ‘bize’ zaidi. Kuhusu mavazi, Misosi nimeshakuwa mtu mzima, ndiyo sababu iliyonifanya nikanyoa rasta zangu,” alisema Misosi.
********

Wednesday, March 18, 2009

JE, UMEWAHI KUFANYA ENEMA?

HAPO zamani, niliwahi kuandika makala kuhusu somo tajwa hapo juu, somo ambalo liligusa wasomaji wengi wa gazeti hili. Katika simu kadhaa ambazo nimekuwa nikipokea kutoka kwa wasomaji wakiomba msaada wa masuala mbalimbali, hujikuta nikilazimika kuwaeleza pia kuhusu suala la Enema, lakini wengi wao wameonekana kutoifahamu.

Hivyo leo nimeamua kuanza kuandika tena mfululizo wa makala haya kuhusu suala hili, ambalo ndilo msingi wa afya bora na uhai wa kila mmoja wetu. Inawezekana hata wewe ukawa unasikia kwa mara yako ya kwanza neno ENEMA, lakini napenda kukuhakikishia kwamba neno hili lipo tangu enzi za mababu zetu na ni maarufu sana miongoni mwa kizazi cha babu au bibi zetu waliyopo hai hivi sasa.

Babu zetu walidumisha sana enema katika maisha yao ya kila siku katika familia nzima, kwa kufanya enema mara kwa mara waliweza kujiepusha na maradhi mengi na kuishi na afya njema, wengine wakiwa wangali hai hadi sasa wakiwa na nguvu zao katika umri wa miaka 80 au 90.
Kwa lugha nyepesi kabisa, Enema ni njia ya asili (natural way) ya kusafisha na kuondoa sumu (cleansing and detoxifying) kwenye utumbo mpana kwa kutumia maji ambayo mtu huyapitisha kupitia sehemu zake za nyuma. Mtu anaweza kujisafisha mwenyewe kwa kutumia vifaa malaumu (Enema Kit) au kwa kwenda kwenye kliniki maalumu, ambazo kwa hapa nchini sijawahi kusikia kama zipo, lakini katika nchi zilizoendelea kliniki za aina hii zipo nyingi.

Njia hii ina wafaa sana wale ambao hawewezi kunywa maji mengi asubuhi kwa utaratibu tuliokwisha ueleza, kwa lengo la kusafisha mifumo yao ya mwili, ukiwemo utumbo mkubwa ambao ndio unaotakiwa kuwa safi wakati wote. Kunywa maji kama tiba, ni njia moja ya kusafisha utumbo wako mkubwa, lakini kama huwezi njia hiyo ya kunywa, basi huna budi kufuata njia hii, lengo likiwa ni kuhakikisha utumbo wako mkubwa unakuwa safi.

KUNA ULAZIMA GANI WA KUFANYA ENEMA?
Katika tasinia hii ya Enema, kuna msemo mmoja maarufu sana usemao Death Begins at the Colon (kifo huanzia kwenye utumbo mkubwa). Msemo huu una maana kwamba chanzo cha maradhi mengi yanayosababisha vifo vya binadamu huanzia kwenye utumbo mkubwa pale unapokuwa mchafu na mazalia ya maradhi.

Inaelezwa na wataalamu wa afya kwamba utumbo mkubwa (large Intestine), unapokuwa mchafu, kila kitu hushindwa kufanya kazi yake ipasavyo, hata kama utakula lishe au virutubisho bora kiasi gani, haviwezi kukusaidia sana kiafya na hata utakapotumia dawa kujitibu na magonjwa, dawa haziwezi kufanya kazi yake sawa sawa, kwani njia zote huwa zimezibwa.

Itaendelea wiki ijayao…


Monday, March 16, 2009

SOFA SET FOR SALE!

IMPORTED BRAND NEW SOFA SET INAUZWA BEI POA, Tshs. 2.2M HUWEZI KUPATA KWA BEI HII SHOWROOM, PIGA SIMU:0717 077451, 0774 770077. ZIPO DAR ES SALAAM, KIJITONYAMA.

WIKIENDA SHOWBIZ!

Beyonce
Nas: AMEWAHI KUWAPITIA BEYONCE, MARY J. BLIGE, FOXY BROWN
Wasomaji na wapenzi wa safu hii waliotutumia meseji kibao, wakitaka kufahamu mkali wa Hip Hop kutoka pande za Marekani, Nas Escoba (pichani juu) amewahi kujiachia na mastaa gani wa kike, leo ndiyo siku yao ya kufurahi kwani hii ndiyo listi ya mchizi huyo.

Unaweza usiamini, lakini kwa mujibu wa mtandao ukweli ni kwamba, Nas amewahi kujirusha na mke wa Jay-Z, Beyonce Knowles, akaja kwa demu wa sasa wa Rick Rosse, Foxy Brown. Mabinti wengi aliyowahi kuwapitia ni pamoja na K.D. Aubert, Karrine Steffans na Tracee Ellis Ross ambaye nyota yake ni Nge.

Mastaa wengine wa kike waliowahi kujirusha na Nas ni pamoja na Carmen Bryan (1992- 2001), Mary J. Blige (1997) na Kelis aliyeanza naye tangu 2005 hadi hii leo. Akiwa na umri wa miaka 35 hivi sasa, mchizi alizaliwa Septemba 14, 1973 katika Jiji la Long Island, Queens, huko New York, Marekani na kupewa jina la Nasir Bin Olu Dara Jones.
******************************

FEROOZ, NATURE KUSIMAMA PAMOJA DIAMOND JUBILEE
Wasanii Juma Kassim ‘Nature’ na Ferouz Mrisho ‘Ferouz’ Ijumaa ya wiki hii, wanatarajia kutambulisha albamu mbili kwa mpigo ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee.

Wakati Nature akitambulisha albamu yenye jina la Tugawane Umasikini, Ferouz atasimama jukwaani na ‘Muziki na vyombo’.
******************************

BABY MADAHA, FEISAL KUSEPA INDIA
Wasanii wawili, Baby Madaha (JUU KULIA) na Feisal waliotambulishwa kupitia Shindano la Bongo Star Search 2007, wanatarajia kutimkia nchini India Machi 18, mwaka huu kwa ajili ya kurekodi video za nyimbo zao, Imelda Mtema anashuka nayo.

Akipiga stori na safu hii Mkurugenzi wa Kampuni ya Pilipili Intertainment, Naresh Dhat ambaye ndiye Meneja wa wasanii hao alisema kuwa, ameamua kuwapeleka wasanii hao India ili kuleta mapinduzi mengine katika game ya muziki wa Bongo Flava.

“Wakiwa India watafanya video za nyimbo mbili ambazo ni ‘Indian Fruits’ wa Baby Madaha na ‘Back it up’ walizoimba kwa kushirikiana, huo ni mwanzo tu, tumeanza na wasanii hao wawili lakini lengo kubwa ni kuwasaidia wengi zaidi ambao hawana uwezo kifedha,” alisema meneja huyo.
*******************************
FLORA KUTAMBULISHA VIDEO MPYA
Kutoka ndani ya sanaa ya muziki wa Injili, msanii Flora Mbasha ameiambia safu hii kwamba, anatarajia kuzindua albamu mpya ya video za nyimbo zake yenye jina la ‘Furaha yako’, siku ya Sikukuu ya Pasaka ikiwa ni zawadi kwa wapenzi wa kazi zake, Ester Sylivester alicheki naye.

Staa huyo wa Injili alisema kuwa, sehemu kubwa ya maandalizi ya uzinduzi huo imeshakamilika na siku chache zijazo atalitaja eneo la tukio itakapofanyika shughuli hiyo.

“Nawaomba wapenzi wa nyimbo zangu na muziki wa Injili kwa ujumla wasikose kununua albamu hiyo ya video pamoja na ‘audio’ yake ili wapate kusikia maneno mazuri ya kumtukuza Mungu niliyoongea ndani ya kazi hizo,” alisema Mbasha ambaye bado anaendelea kutamba na nyimbo zake mbalimbali katika fani hiyo.
*****************************

Dar es Salaam Put Your Hands Up inakuja
'Dar es Salaam Put Your Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu) ni bonge la mpambano litawahusu wasanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka ndani ya Wilaya tatu za Jiji hilo la Dar, ambalo linaendeshwa na gazeti ndugu, Ijumaa, linalotoka kila siku ya Ijumaa.

Mpambano huo una lengo la kutafuta wilaya moja yenye wasanii wakali na utawahusisha mastaa kutoka pande za Ilala, Kinondoni na Temeke, mwisho wa siku itatajwa iliyoibuka na ushindi.

Kwa kuanza, wewe msomaji unatakiwa ututumie majina ya wasanii kutoka katika Wilaya ya Kinondoni ambao unadhani wataiwakilisha vyema sehemu yao kunako shindano hili. Andika ujumbe mfupi (SMS) ukilitaja jina la msanii kutoka Kinondoni ambaye unadhani anastahili kuiwakilisha wilaya yake, kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Mwisho wa kupokea kura yako ni Jumatano mchana wiki hii.
***********************************

Sunday, March 15, 2009

SPECIAL OFFER FOR LADIES!




VIATU: 40,000/= TU
BIKINI: 5,000/= TU

JUST CALL: 0713 834249

PICHA INA ONGEA MANENO 1000!

.....hakipiti kitu hapa!!!

..safari ni safari tu

...ukibanwa sana, umeme sometimes si lolote!

picha zaidi hapa

Friday, March 13, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!

Witness na ndoto za ‘Wakilisha’
Msanii Witness Kaijage ambaye ni mmoja kati ya vijana watatu waliokuwa wanaunda Kundi la Wakilisha kabla halijasambaratika, amesema na ShowBiz kwamba anatamani siku moja ‘cruu’ yao hiyo irudi katika game ili heshima iendelee kuwepo. Edna Katabalo alicheki nae.

“Licha ya kubanwa na majukumu ya hapa na pale, naamini siku moja ‘Wakilisha’ itarudi tena katika gemu, hiki ndicho kitu ambacho nataka mashabiki wetu wafahamu. Kundi lipo, kilichotutenganisha ni harakati za kutafuta maisha,” alisema Witness.
**********
Nyoshi: Sina bifu na Ndanda Kosovo
Kiongozi wa Bendi ya FM Academia, Nyoshi El Saadat, amesema na ShowBiz kwamba hana bifu na mwanamuziki Ndanda Kosovo kama ilivyowahi kuripotiwa hivi karibuni na baadhi ya vyombo vya habari, Rhobi Chacha alicheki nae.

Ndani ya safu hii, Nyoshi alisema kuwa hawezi kuwa na ugomvi na Mkongomani mwenzake huyo wala mwanamuziki wa bendi yoyote hapa nchini, bali watu wanaoeneza uvumi huo wanalengo la kumchafua.“Nadhani kuna watu wanaeneza maneno hayo kwa lengo la kunichafua ili jamii inione mimi ni mkorofi,” alisema Nyoshi.
********
Suma G Aibukia pande za Masaki
Kutoka ndani ya Familia ya Hot Pot, iliyopiga kambi pande za Karataka, Dar es Salaam, msanii Suma G ambaye alipotea kwa muda ndani ya game ya muziki wa kizazi kipya ameibukia ndani ya studio za MJ, zilizopo Masaki, Dar es Salaam ambako anapigia kazi hivi sasa.

Akipiga stori na ShowBiz, mchizi alisema kwamba ukimya wake ulikuwa ni wa kujipanga, sasa amepangika na kuibukia kunako studio hizo ambako anapiga kazi na mtayarishaji Maco Chali, kabla ya kuachia ngoma yake mpya yenye jina la ‘Silaha maneno’.

“Kaka huo ni ujio mwingine, ngoma hiyo itatambulisha albamu yangu mpya ambayo nimewapa shavu mastaa kibao kama Fid Q, Nature, Chegge, Hardmad na wengine kibao,” alisema Suma G.

******************************************

Dar es Salaam: Put Your Hands- UP
Baada ya kukamilika kwa mpambano wa kumtafuta staa wa kike mwenye mvuto wa kimapenzi, ‘Ijumaa Sexiest Girl’ ambapo mrembo Irene Uwoya aliibuka na ushindi, ShowBiz inakuletea bonge la shindano lingine, ‘Dar es Salaam Put Your Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu) ambalo litawahusu wasanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka ndani ya wilaya tatu za jiji hili.

Mpambano huo una lengo la kutafuta wilaya moja yenye wasanii wakali na utawahusisha mastaa kutoka pande za Ilala, Kinondoni na Temeke, mwisho wa siku, itatajwa iliyoibuka kidedea kama ilivyokuwa kwenye mashindano yaliyopita ndani ya gazeti hili.

Kwa kuanza, wewe msomaji unatakiwa ututumie majina ya wasanii kutoka katika Wilaya ya Kinondoni ambao unadhani wataiwakilisha vyema sehemu yao kunako shindano hili. Tumefanya hivyo kwa kuwa kila wilaya ina wasanii wengi na hatuwezi kuwaweka wote kutokana na ufinyu wa nafasi.

Andika ujumbe mfupi (SMS) kwenye simu yako ya mkononi ukilitaja jina la msanii kutoka Kinondoni ambaye unadhani anastahili kuiwakilisha wilaya yake, kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Wiki ijayo tutazitoa picha na majina ya wasanii watakaotajwa kabla ya kuendelea kuwatafuta wakali wa Ilala na Temeke.
*****

Tuesday, March 10, 2009

Epuka ugonjwa wa moyo kwa kula hivi:


KILA mara tunasisitiza kuwa chakula ndiyo kila kitu katika maisha yetu, pale tunapokitumia vizuri kinatuletea faida na pale tunapokitumia vibaya hutuletea madhara makubwa katika afya zetu, yakiwemo matatizo ya ugonjwa wa moyo.

Utafiti uliofanywa nchini Marekani hivi karibuni, unaonesha kuwa, takriban Wamarekani Milioni 9 wanasumbuliwa na ugonjwa wa moyo na unaua mtu mmoja kila baada ya sekunde 37! Sijajua hali ikoje nchini Tanzania.

Ili kujiepusha na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo, mambo 10 yafuatayo hayana budi kufuatwa na kuzingatiwa:

KIJUE KIWANGO CHAKO CHA KOLESTRO
Kwa kawaida binadamu tuna mafuta mwilini yanayojulikana kitaalamu kama ‘High-density Cholesterol (HDL), Low-Density Cholesterol (LDL) na Triglycerides (TG). ‘LDL’ na ‘Triglycerides’ ni mabaya na hasa ukiwa nayo mengi mwilini, ndiyo huwa chanzo cha ugonjwa wa moyo. Hivyo ni vyema ukaenda kwa Daktari na kujipima afya yako.

JIJUE UKO KATIKA HATARI KIASI GANI
Utakuwa uko katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo iwapo utakuwa na matatizo ya presha, kiwango kikubwa cha mafuta mabaya ya kolestro na ukawa unavuta sigara pia. Wataalamu wetu wanatuambia kuwa matatizo hayo yana muongezea mtu hatari ya kupata ugonjwa wa moyo mara nane zaidi katika kipindi cha miaka sita ijayo, hivyo epuka uvutaji sigara.

PUNGUZA UZITO
Kupunguza uzito, hata kwa kilo 5, ni jambo la lazima iwapo unataka kujiepusha na magonjwa ya moyo. Uzito mkubwa sana ndiyo huwa chanzo kikuu cha magonjwa ya kisukari, shinikizo la damu ambayo hatimaye huweza kusababisha ugonjwa wa moyo.
PUNGUZA ULAJI WA MAFUTA
Vitu kama siagi, krimu, ‘mayonaizi’ na vipande vya nyama vyenye mafuta ni miongoni mwa yale mafuta mabaya (“bad” LDL cholesterol), ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa uzibaji wa mishipa ya damu (arteries) mwilini, hivyo epuka ulaji wa vitu hivyo kwa wingi. Badala yake kula mafuta yatokanayo na mboga, kula samaki au nyama ya kuku isiyokuwa na mafuta.

ACHANA NA VYAKULA VYA MAKOPO
Kwa kawaida vyakula vya makopo huwa na mafuta na chumvi nyingi pamoja na kemikali nyingine za kuhifadhia chakula ambavyo huchangia mlaji kuwa na mafuta mabaya mengi mwilini. Ununuapo vyakula kwenye makopo, lazima usome na ujue vilivyomo kabla ya kuamua kutumia.
KULA VYAKULA VYENYE ‘Fiber’
Kwa Kiswahili ‘fiber’ inajulikana kwa jina la ‘ufumwele’ ambao ni muhimu sana kwa ustawi wa moyo. Tunashauriwa kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha ufumwele, kama vile maharage, kunde, n.k pamoja na matunda jamii ya machungwa.

KULA NAFAKA HALISI
Badala ya kupenda kula vyakula vilivyotengenezwa kutokana na nafaka zilizokobolewa, ambazo huwa chanzo cha magonjwa kama kisukari na presha, kama vile mkate au ugali mweupe, pendelea kula sembe, dona au mkate mweusi ambao husaidia kuondoa mafuta mabaya mwilini na huepusha magonjwa ya kisukari.

KULA SAMAKI
Utafiti unaonesha kuwa mtu akila samaki, angalau mara mbili kwa wiki, anajiepusha na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kwa asilimia 30 zaidi. Samaki wana mafuta aina ya Omega-3 ambayo hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini yanayosababisha kuziba kwa mishipa ya damu. Pia Omega- 3 hupunguza kiwango cha presha ya damu mwilini.

KULA ‘NJUGU’
Utafiti mwingine unaonesha pia kuwa watu wanaopenda kula ‘njugu’, kama vile karanga, korosho ,n.k, kwa wiki mara mbili au nne, wana uwezekano mdogo sana wa kupatwa na magonjwa ya moyo kuliko watu wasiokula. ‘Njugu’ zina aina nzuri ya mafuta kwa afya ya moyo.

‘KUNYWA’ KIASI
Utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa wanywaji kiasi wa kilevi, wana uwezekano mdogo wa kupatwa na ugonjwa wa moyo kuliko wasiokunywa kabisa. Kilevi- hasa wine- kinasadikika kuifanya damu kuwa nyepesi na kuongeza mafuta mazuri mwilini (HDL Cholestrol).

Zingatia mambo hayo 10 na moyo wako utakuwa salama!

Monday, March 9, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Bushoke, Ngwea watimkia chuoni Bagamoyo
Baada ya ziara ndefu kwa ajili ya kuinadi albamu yake mpya, ‘Dunia njia’, msanii Rutta Maximilian Bushoke na mchizi aliyekuwa naye bega kwa bega kwenye uzinduzi huo, Albert Mangwea ‘Ngwea’ wameamua kujitupa pande za Chuo cha Sanaa, Bagamoyo kwa ajili ya kuongeza maujanja zaidi katika game yao ya muziki, Edna Katabalo alipiga naye stori.

Akipiga stori na safu hii, Bushoke alisema kuwa yeye na Ngwea wameamua kurudi darasani kunako chuo hicho ili waweze kuongeza ufahamu zaidi katika sanaa ya muziki ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na ushindani uliopo kwenye tasnia hiyo hivi sasa, kwani wanaamini kwamba, bila elimu huwezi kufika kimataifa zaidi.

“Tumegundua kwamba bila elimu hatuwezi kufanya mambo kwa ufanisi zaidi, ndiyo maana mimi na Ngwea tumeamua kuja hapa Chuo cha Sanaa Bagamoyo ili kujiongezea maujuzi zaidi. Hata kama utakuwa juu kwenye sanaa ya muziki huwezi kujua kila kitu, itafikia kipindi lazima ujifunze,” alisema Bushoke.

Aidha, Bushoke alisema kwamba, wakiwa chuoni hapo watapiga kozi fupi ya miezi mitatu, kabla ya kutunukiwa vyeti ambavyo vitatambulika na chuo hicho.
***********************************************

Jordin Sparks: hawa ndiyo wanaume aliojirUsha nao
Mkali wa muziki wa Pop kutoka pande za Obama (Marekani), Jordin Sparks ambaye hivi sasa yuko juu kupitia ngoma kadhaa kama ‘Step At a Time na No Air aliyoigonga na Chriss Brown, ndiye staa tunayedondoka naye kupitia safu hii, ‘Ebwana Dah!’, baada ya kupata meseji za kutosha kutoka kwa wasomaji na wapenzi wa msanii huyo.

Kwa mujibu wa kale kamtandao ketu, Jordin Sparks hana listi ndefu ya mastaa wa kiume aliyowahi kujiachia nao kama ilivyokuwa kwa wasanii wengine waliyopita kunako ‘Ebwana Dah!. Mastaa wa kiume waliyowahi kula raha na binti huyo mwenye umri wa miaka 19 hivi sasa ni pamoja na Steph Jones (2004-2008), Chris Richardson (2007-2008) na Blake Lewis (2008).

Jordin Brianna Sparks ambaye ana urefu wa futi sita na macho ya rangi ya Dark Brown, huku nyota yake ikiwa ni Nge, alizaliwa Desemba 22, 1989 huko Phoenix, Arizona, Marekani. Kwa ishu zaidi kuhusu yeye mcheki kupitia www.jordinsparks.com. Wewe msomaji, unatamani kufahamu uhusiano wa zamani wa staa yupi? Tuandikie ujumbe kupitia simu 0715-110 173.
*****************************

Witness: Wasanii tuache utovu wa nidhamu
Mshindi wa tuzo ya ‘Channel O’ mwaka jana, kupitia ngoma yake yenye jina la ‘Ziro’, Witness Kaijage amesema na safu hii kwamba, anasikitishwa na tabia za utovu wa nidhamu zikiwemo kuvuta bangi, fujo na vitendo vya ngono vinavyofanywa na baadhi ya wasanii kwani zinapoteza imani kwa mashabiki na wadau wa game hiyo, cheki na Edna Katabalo kwa stori zaidi.

Msanii huyo ambaye ni miongoni mwa wasichana wachache wanaokomaa kunako game ya muziki wa Hip Hop, pia anakerwa na kitendo cha baadhi ya wasanii wa Kibongo kuigana staili, yeye anaamini kwamba msanii hakuna haja ya kuwa kama fulani ili atoke, zaidi ni kufanya kazi kwa bidii.

“Nawaomba wasanii wenzangu waachane na tabia hizo, wabadilike ili kuifanya kazi yetu ya muziki iheshimike zaidi kama kazi nyingine. Nachojua mimi ni kwamba kujituma na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ndiyo silaa kubwa ya mafanikio, kila msanii anatakiwa ajiheshimu,” alisema Witness.

Hivi sasa staa huyo aliyekuwa akiunda kundi la Wakilisha yupo kwenye maandalizi ya mwisho ya ngoma yake mpya, ‘Attention Please’ ambayo itadondoka kunako vituo vya redio na televisheni mwishoni wa mwezi huu.

*****************