Saturday, September 1, 2007

ZE COMEDY MATATANI!


Na Mwandishi Wetu

Kikundi maarufu cha sanaa za uchekeshaji kijulikanacho kwa jina la Ze Comedy cha jijini Dar es Salaam kiko matatani baada ya kudhihaki maadiko takatifu ya dini ya kiislamu (kurani), hivyo kuwatibua waislamu nchini.

Aidha wasanii hao wametakiwa kuwaomba radhi waislamu kabla hawajachukuliwa hatua kali ambayo huenda ikawadhuru.

Onyo hilo limetolewa na Sheikh Hashim Ruseganya wa Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam wakati wa hotuba ya swala ya Ijumaa aliyoitoa msikini hapo hivi karibuni. (udaku zaidi: http://www.globalpublisherstz.com/risasijumamosi/)

Thursday, August 30, 2007

RAY MBARONI CHINA


Na Kulwa Mwaibale
Mkali wa filamu na Michezo ya kuigiza nchini, Vincent Kigosi 'Ray', hivi karibuni alionja joto ya jiwe baada ya kutiwa mbaroni na Askari Polisi wa China.

Chanzo chetu cha habari kilichopo nchini humo, kinaeleza kuwa wanausalama hao walifikia hatua hiyo baada ya kumhisi kuwa alikuwa akitaka kufanya ugaidi.

Aidha chanzo hicho ambacho hakikupenda kuandikwa jina lake gazetini, kilieleza kuwa Ray alifika nchini humo akiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Tollywood Movie, Eric Shigongo, kwa kazi ya kurudufu filamu ya Fake Pastors.

"Mimi nilikuwa mwenyeji wao, walikuja kwa ajili ya kurudufu filamu hiyo ili waweze kuiuza kwa bei nafuu Tanzania, lakini wakiwa hapa wakapata mkataba na kampuni nyingine kwa ajili ya kutengeneza filamu moja”, kilisema chanzo hicho.

Habari zaidi zinasema, Ray aliingia mkataba na Kampuni ya Chinese Film Production kwa niaba ya Kampuni ya Tollywood Movie ya nchini Tanzania kwa makubaliano ya kutengeneza filamu moja iliyopewa jina la From China With Love.

Kati ya wasanii ambao wameshiriki katika filamu hiyo kutoka China ni pamoja na mwanamuziki maarufu Irene Maltino ambaye ni raia wa Ufilipino anayefanya shughuli zake za muziki nchini humo.

"Baada ya kuwapata wasanii hao, wapiga-picha wa Kampuni ya Chinese Film Production wakiwa na Ray na mastaa hao, walikwenda ufukweni usiku kupiga picha za filamu hiyo," kilieleza chanzo hicho.

Habari zaidi zinaeleza kuwa wakiwa ufukweni hapo wakiendelea na zoezi la upigaji picha, polisi walifika na kuwatia mbaroni ambapo waliwahoji na kumtaka Ray aoneshe kibali cha kupiga picha na hati yake ya kusafiria, vitu ambavyo hakuwa navyo, hali iliyosababisha Ray kufikishwa kituoni.

"Alipokuwa kituoni alimpigia simu Mkurugenzi wake (Eric Shigongo) ambaye alikwenda kuchukua hati ya kusafiria pamoja na kibali katika hoteli waliyofikia, kisha akavipeleka polisi ambapo aliachiwa," kilihitimisha chanzo hicho.

Akizungumza na Ijumaa baada ya kuwasili nchini, Ray alikiri kukamatwa na askari nchini China ambao walifikiri alikuwa akipiga picha hizo kwa nia ya kufanya uhalifu, lakini walipogundua sivyo walimwachia.

"Ni kweli kaka, nilipatwa na dhoruba kidogo lakini baadaye waliniachia huru! Unajua nilikosea kitu kimoja tu, kutembea bila hati yangu na kibali cha kupiga picha, kama ningekuwa navyo nisingepata usumbufu huo. Hata hivyo kila kitu kilikwenda sawa, namshukuru Mungu nimerudi nyumbani salama salimin," alisema Ray.

HII NI KASHESHE!


Na Richard Bukos
Mama mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Cecilia hivi karibuni alijikuta akipata kipondo cha nguvu baada ya kufumwa akila raha na mume wa jirani yake.

Tukio hilo la aibu lilitokea usiku wa manane wa Agosti 28 mwaka huu katika kilabu cha pombe za kienyeji kilichopo Manzese karibu na Uwanja wa Fisi jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, habari za dada huyo kufumaniwa na kupewa kisago zilitokana na kuvuja kwa siri ya ‘kumchuna’ na kufanya mapenzi na mume wa mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la mama Jane.

Ilidaiwa kuwa, mume wa mwanamke huyo ambaye jina lake halikupatikana alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na kimwana mwingine na kwamba alikuwa akikutana naye usiku na kuponda raha kwenye kilabu hicho.

Siku hiyo ya tukio wagoni hao wakiwa katika mkao wa hasara, mke wa mwanaume huyo alitokea ghafla na kuanza kumtembezea kipigo, jambo lililoashiria kuwa alikuwa akimvizia mbaya wake.

Akionekana kujawa na hasira baada ya kuwabamba mama Jane alisikika akisema, “Si ulikuwa unakataa” alikatiza usemi wake na kumkunja mbaya wake huku akimwacha mumewe akitoweka kiaina.

Ghafla kilabu hicho kiligeuka uwanja wa ngumi na mieleka, huku mpambano ukimwelemea mgoni aliyeonekana kuyatungika ‘matap tap’ ya ofa ya mume wa mtu.

Hata hivyo baadhi ya wakata kilevi waliokuwa eneo hilo la tukio hawakuonesha kujali kwa kuamulia ugomvi huo, badala yake walisisitiza wagomvi waachwe wafundishane adabu.

Aidha baada ya sakata hilo kufikia tamati mama Jane alimwambia mwandishi wetu kuwa habari za kuibiwa mume alikuwa nazo siku nyingi na kwamba alikuwa akiwafuatilia ili awanase laivu.

“Nilikuwa na taarifa kuwa huyu ****** anatembea na mume wangu lakini nikawa sina uhakika, leo ndio nikaweka mtego wangu na bahati nzuri nimewabamba laivu,”alisema mwanamke huyo.

Aliongeza kuwa kwa tukio hilo ndiyo mwisho wa maisha yake ya ndoa kwani hawezi kuishi na mwanaume mhuni katika zama hizi za ugonjwa hatari wa UKIMWI.
(zaidi bonyeza hapa:http://www.globalpublisherstz.com/amani/)

Wednesday, August 29, 2007

Niue nsiue?


Na Mwandishi Wetu
Mwanamke mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, hivi karibuni alikumbwa na balaa la aina yake baada ya kupigwa vibaya kisha kuvuliwa nguo na kijana anayedaiwa kuwa ni mumewe.

Tukio hilo lilitokea saa 9.00 usiku, Jumamosi iliyopita katika eneo la Ukumbi wa disco wa Kahama Centre, uliopo Tarafa ya Makere mkoani Kigoma.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ambacho kilikuwepo katika eneo la tukio, dada huyo aliiingia katika ukumbi huo kwa ajili ya kwenda kucheza disco bila kumfahamisha mumewe.
Habari zinasema kuwa akiwa ndani ya ukumbi huyo, alitongozwa na kijana mmoja ambapo alimkubalia na kupanga kutoka naye mara baada ya kumalizika kwa muziki.

Pamoja na makubaliano hayo, kijana huyo alimpatia mwanamke huyo shilingi 2,000 kama kichocheo pamoja na kumnunulia vinywaji ili asimwangushe.

Habari zaidi zinasema kuwa muziki ulipoisha, kijana huyo alimfuata dada huyo na kutaka waondoke, lakini alishangaa alipoambiwa kuwa hamjui.

Chanzo hicho kilisema kauli ya kutomtambua kijana huyo ilitokana na taarifa alizopewa msichana huyo kuwa mumewe alikuwa ametinga ukumbini hapo kumsaka.

“Sababu hasa ya kugoma kuondoka na kijana huyo ni baada ya kupata taarifa kuwa mumewe alikuwemo ndani ya ukumbi huo akimvizia baada ya kutonywa na wasamaria wema ,” kilisema chanzo hicho.

Habari zinasema kuwa muda mfupi baada ya mzozo, mume wa kijana huyo alifika sehemu walipokuwa wamesimama na kuwafuma wakibishana huku mwanamke huyo akidaiwa pombe aliyoinywa na shilingi 2,000 alizopokea.

Habari zaidi zinasema kuwa, mume huyo alimkamata kijana aliyekuwa na mkewe na kabla ya kumtandika makonde alichurupuka na kukimbia kusikojulikana.

“Kuona hivyo, mwanaume huyo alimgeukia mkewe na kumkwida huku akimpiga na kumlazimisha amtaje kijana aliyekuwa naye usiku huo,” kilisema hicho.

Kipigo hicho kiliendea kwa takriban dakika kumi ambapo alimshika msichana huyo na kumtoa nje kwa nguvu huku akimvua nguo zake na kubaki uchi.

Alipomfikisha nje aliendelea kumpa kisago huku akitoa maneno ya kashfa kwa kuwauliza watu waliokuwa wakishuhudia songombingo hilo; ‘niue ‘nsiue?’.

Habari zinasema kuwa kipigo kilipomzidi, dada huyo alidondoka chini na kugalagazwa kwenye mchanga, ambapo mmoja kati ya watu walioshuhudia aliweza kumpiga picha (kama inavyoonekana ukurasa wa mbele wa gazeti hili).

Chanzo cha habari kilisema kuwa msichana huyo aliokolewa na wasamaria wema baada ya kuona anaendelea kudhalilishwa.

Mwanamke huyo aliingizwa kwenye gari ya kukodi na kuondoka, haikufahamika alikopelekwa kwani mumewe alionekana akiranda sehemu hiyo kumsaka mbaya wake.

Habari zaidi zinasema kuwa tukio hilo limeacha gumzo kubwa mtaani hapo ambapo baadhi ya watu walikuwa wakimuonea huruma mwanamke huyo huku wengine wakisema alistahili kichapo kutokana na tabia aliyoionyesha.

Habari zaidi: http://www.globalpublisherstz.com/risasimchanganyiko/

Tuesday, August 28, 2007

YOU ARE WHAT YOU EAT


Tufaha(Apple): Tunda lingine lenye maajabu mwilini!

Tumerudi tena kwenye makala za uchambuzi wa faida za matunda mwilini na leo hii tunalichmbua tunda maarufu la Tufaha au wengi wanalijua kwa jina la epo (apple).Tunda hili ni miongoni mwa matunda ghali na kwa kawaida huingizwa nchini kwa wingi kutoka Afrika Kusini. Wastani wa bei ya tunda hili jijini Dar es salaam ni shilingi 400 kwa tunda moja sazi ya ngumi ya mtoto.

FAIDA ZA TUFAHA KIAFYA

Utafiti wa hivi karibuni kuhusu tunda hili, umethibitisha kuwa ule msemo wa kiingereza wa siku nyingi usemao An Apple A day keeps the doctor away (tunda moja kwa siku humuweka daktari mbali nawe) ni wa kweli kwani kuna virutubisho muhimu vya Fiber, Flavonoids, na Fructose-translate ambavyo hutuweka katika afya njema.

Kwa mujibu wa watafiti wa tunda hili, mtu akila shufaa moja na maganda yake anapata kiasi kisichopungua gramu 3 za kirutubisho aina ya fiber (ufumwele), kiasi ambacho ni kikubwa kwa asilimia 5 zaidi ya kile kinachopendekezwa na wataalamu mtu kula kwa siku. Na faida za kirutubisho hizi ni nyingi.

Baadhi ya faida kubwa na za msingi za kirutubisho hicho katika mwili wa binadamu, ni uwezo wake mkubwa wa kuteketeza kabisa kiasi cha mafuta mabaya mwilini (cholestrol levels), kuondoa hatari ya kuziba kwa mishipa ya damu, kupatwa na mshituko wa moyo na kiharusi.

Kwa maana nyingine ukiwa mlaji mzuri wa tunda hili, utajiepusha kwa kiwango kikubwa na matatizo ya shinikizo la damu au kupatwa na kiharusi (stroke), matatizo ya kiafya ambayo katika maisha ya siku hizi yamekuwa ni ya kawaida na watu wengine huyahusisha na imani za kishirikina.

Aidha epo linasifika kwa kuwa askari mzuri wa kupambana na matatizo ya tumbo, kama vile kujaa gesi, kuharisha, kukosa choo kwa muda mrefu na matatizo mengine kama hayo. Mtu mwenye matatizo hayo anapolila tunda hilo, basi hupata ahueni haraka na kama huna matatizo hayo, basi utakuwa unajitengenezea kinga madhubuti.

Utafiti mwingine kuhusu tunda hili, umeonesha kuwa epo linasaidia katika kuongeza kinga ya mwili na kinga dhidi ya saratani mbalimbali za mwilini kutokana na kuwa na kiwango kikubwa sana cha kirutubisho aina ya Flavonoids.

TUNDA ZURI KWA WAGONJWA WA KISUKARI

Epo lina kiasi fulani cha sukari ya asili, ambayo ni nzuri kwa watu wenye ungonjwa wa kisukari, kwani inapochanganyika na kirutubisho aina ya fiber husadia sana kuweka kiwango cha sukari mwilini katika hali inayotakiwa.

HUZUIA MAWE KWENYE FIGO

Kama unataka kupata kinga madhubuti dhidi ya ugonjwa wa mawe kweye figo (kidney stones), basi kunywa juisi ya epo. Utafiti uliochapishwa hivi karibuni kwenye jarida la masula ya lishe la Uingereza (British Journal of Nutrition), umeonesha kwamba, kwa kunywa nusu au lita moja ya juisi ya epo kila siku, unaondoa uwezekano kabisa wa kupatwa na tatizo hilo ambalo hujitengeneza lenyewe kwenye figo.

Kwa ujumla ulaji wa epo na matunda mengine, kuna faida sana katika mwili wa binadamu na kunaepusha mwili kupatwa na maradhi ya mara kwa mara. Hatuna budi kuheshimu ushauri tunaopewa na wataalamu wetu kama kweli tunajali afya zetu.

HATARI!

Na Mwansishi wetu
Kitendo cha baadhi ya wabunge vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania kulipua mabomu imeelezwa kuwa ni hatari kwa maisha yao.

Wakizungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi waliohojiwa jijini Dar es Salaam walisema kuwa asilimia kubwa ya vigogo wanaodaiwa kuhusika na kashfa mbalimbali mara nyingi hawapendi kutajwa majina yao, hivyo hujenga chuki kwa wale wabunge wanaowataja wakati wa kulipua mabomu.

Aidha Bw. Abdallah Juma mkazi wa Mikocheni alisema kuwa marehemu Amina Chifupa alipokuwa amelivalia njuga suala la dawa za kulevya bungeni kuwa kuna baadhi ya vigogo wanaohusika na biashara hiyo walimuona kama adui.

"Amina alifungua njia baada ya kuanza kufichua maovu mbele ya jamii yanayofanywa na watu wachache bila kujali maslahi ya Taifa lakini alipata vitisho baadaye alifariki dunia kwa kifo cha kutatanisha bila kuwataja vigogo hao hadharani ingawa alisema alikuwa na orodha ndefu ya wahusika," alisema Bw. Juma.

Aliendelea kusema kuwa Mhe. Zitto Kabwe ambaye alilitaka bunge liunde tume ya kuchunguza usainishwaji wa mkataba wa madini huko Uingereza uliofanywa na Waziri wa Nishati na Madini Bw. Nazir Karamagi alijikuta akifungiwa kwa kipindi cha miezi mitano kutojihusisha na shughuli za bunge hali iliyolalamikiwa na watu wengi.

Naye Mhadhiri mmoja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini alisema kuwa sasa umefika wakati Bunge kusikiliza hoja na kuzifanyia kazi kwa maslahi ya taifa badala ya kuingiza itikadi za kisiasa.

Aliongeza kwa kusema kuwa endapo hoja za msingi zinazotolewa bungeni hazitaangaliwa kuwa ni mbunge wa chama gani katoa, nchi itapiga hatua kimaendeleo.

Akielezea sakata la Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Karamagi juu ya utiaji saini wa mkataba wa madini Uingereza, mhadhiri huyo alisema kunahitajika uchunguzi wa kina ambao utawatoa wananchi wasiwasi na kubaini nani ni mkweli kati yake na Mhe. Kabwe.

“Endapo madai ya Mhe. Kabwe yatafanyiwa kazi na kubainika kuwa yana ukweli basi Waziri Karamagi atakuwa mashakani kupoteza nafasi yake ya uongozi ingawa uamuzi wa mwisho juu ya suala hilo utakuwa mikononi mwa Rais Jakaya Kikwete" alisema mhadhiri huyo.

Mhadhiri huyo alisema kuwa siku hizi inaonekana kuwa ni jambo la hatari kwa waheshimiwa wabunge kutoa hoja nzito zinazohitaji ufafanuzi kwani wengi waliojaribu kufanya hivyo wamepata misukosuko na wengine hata kutishiwa maisha yao.

Wakati huo huo, marafiki na ndugu wa karibu wa Bw. Mohamedi Mpakanjia wamekuwa wakimuombea apone haraka ili arudi kushirikiana na jamii katika masuala ya maendeleo.

Aidha rafiki yake mkubwa, Kapteni John Komba alisema juzi kuwa kitendo cha mtu kuvumisha kuwa Mpakanjia amefariki kilisababisha mshituko mkubwa kwa watu mbalimbali bila sababu za msingi.

" Kitendo hicho si cha kiungwana na nashindwa kujua mtu huyo alikuwa na nia gani, imenisikitisha sana, napenda watu waelewe kuwa Medi hajafa na yupo Hospitali ya Lugalo akitibiwa. Ana matatizo ya kisaikolojia," alisema Komba.

Naye Dk. Maneno Tamba ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Mpakanjia aliliambia gazeti hili juzi kwa njia ya simu kuwa mgonjwa anaendelea vizuri tofauti na mwanzo alipofikishwa hospitalini hapo.
(habari nyingine bonyeza hapa: http://www.globalpublisherstz.com/index.php)

Monday, August 27, 2007

WASANII WA BONGO FLAVA NA TAIFA STARS!

Hivi sasa karibu kila kona ya Bongo, gumzo kubwa ni mechi kati ya timu yetu ya Taifa na Msumbuji ambayo inatarajiwa kupigwa Septemba 8, mwaka huu ndani ya uwanja mpya wa Taifa, sisi kama Abby Cool & MC George Over The Weekend, kupitia kitengo hiki cha ÔStreet VersionÕ hatupo nyuma katika kuonesha uzalendo.

Wanaharakati ya safu hii waliingia mtaani ili na kupiga stori na watu wawili watatu ambao majina yao yanajulikana kwa sana katika jamii yetu. Kikubwa ilichokuwa inataka iwaletee wasomaji ni kauli za mastaa hao ambao kwa nyakati tofauti waliulizwa kwamba ÔWewe kama Mtanzania una maoni gani kuhusu mechi kati ya Stars na Msumbiji?. Haya ndiyo maoni yao:

Jina:Khadija Shabani (K-Sher- (PICHANI JUU)
Maoni: Japo siko karibu sana na mambo ya michezo, napenda kuwaambia Watanzania wenzangu kwamba, sisi kama wazawa tuwe kitu kimoja katika kushangilia na kuhakikisha Stars inafanikiwa kuishinda Msumbiji na kuendelea na michezo mingine huko mbele.
Kwa sababu ushindi huo ni sifa kwa taifa zima, siyo mtu mmoja. Niko pamoja na timu yetu
Jina: Said Fella (Mkubwa)
Maoni: Nikiwa kama Mtanzania, wananchi tuwe wamoja, tuombe Mungu apokee dua zetu ili vijana waende Ghana, kwani kwenda huko ni kufungua soko jipya la mpira na kumuenzi Rais mstaafu, Mkapa na uwanja wetu mpya, kumpa moyo Rais Kikwete kwa kuwapa moyo wachezaji mpaka hapo walipo sasa. Vilevile wachezaji wakaze buti, wasituangushe kwani wakicheza vizuri ni maisha mazuri kwao na taifa kulitangaza na kushangilia.

Jina: Abdul Sykes (Dully Sykes)
Maoni: Mi sina cha zaidi cha kuongelea, ila timu yetu naiamini, nategemea ushindi na si kitu kingine.

Jina: Gervas Kasiga (Chuma)
Maoni: Kikubwa Watanzania wote kuwa na uzalendo kwenye mechi hii, tufute itikadi zetu za kisiasa, kiimani na kitimu. Ushindi kwetu uwe ni wa lazima ili walau tuweze kujiliwaza na ugumu wa maisha unaotuandama, tukumbuke ushindi wa Stars kwa namna moja utakuwa umeongeza nafasi za ajira kwa Watanzania wengi, hususasi wale wote wajasiriamali watakaojiusisha na mauzo ya jezi za Stars, bahati nasibu, documentary, naimani kubwa na wachezaji kwa sababu serikali imeshawajenga, hivyo Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya wao tayari wanayo. Tunachohitaji kwao ni ushindi.

Jina: Selemani Msindi Afande Sele (PICHANI JUU)
Maoni: Mimi naamini timu iko bomba kutokana na mabadiliko makubwa wanayoonesha uwanjani, ukilinganisha na zamani, halafu uzalendo wa Rais JK katika timu pia ni nusu ya kushinda. Ila kocha bado anaweza kuongeza wachezaji kama Machupa, Pawasa, Mrisho Ngasa kuipa nguvu ya ushindi wa uhakika kwa kuzingatia matokeo mabovu tuliyoyapata katika ziara ya Denmark ingawa tunacheza na timu za kawaida kama vile Ghana walivyocheza na Brazil. Watu wanahitaji furaha kupitia kwa timu hiyo, kocha asipuuze mawazo ya wataalam wetu, wazalendo na makocha wa zamani

MEDDY MPAKA NJIA!


Na Waandishi Wetu

Uvumi kuwa mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Mpakanjia amefariki dunia, umezua vilio kila kona ya nchi huku baadhi ya ndugu na marafiki zake wakikusanyika nyumbani kwake wakidhani kuna msiba.

Vilio hivyo, vilitawala sambamba na ndugu pamoja na marafiki wa Mpakanjia kumiminika nyumbani kwa mfanyabiashara huyo, Jumamosi iliyopita, baada ya uzushi kuzagaa kuwa amefariki dunia.

Ndugu mmoja wa Mpakanjia ambaye aliomba hifadhi ya jina lake gazetini, aliliambia Ijumaa Wikienda kwa njia ya simu juzi kuwa, familia ya mfanyabiashara huyo imehuzunishwa na habari hizo za uzushi.

“Hapa tupo nyumbani kwa Medi (Mpakanjia), baadhi ya watu wamekusanyika wanadhani kuna msiba, wanalia sana, hawatuamini tukiwaambia kuwa Medi hajafa, isipokuwa ni kweli anaumwa.

“Kimsingi kuna watu wabaya wanamchuria ndugu yetu, hatujui watapata maslahi gani Medi akifa,” alisema ndugu huyo kwa uchungu.

Aidha, ndugu huyo alisema, uzushi wa namna hiyo ulijitokeza hata kwa aliyekuwa mke wa Mpakanjia, Marehemu Amina Chifupa kabla hajafa, kwani baadhi ya watu walianza kumchuria kifo mapema.

Kufuatia habari hizo za Mpakanjia kufa, watu mbalimbali walilipigia simu gazeti hili, wengine wakilitumia ujumbe mfupi wa maneno (sms), wakitaka kupata uhakika huku baadhi yao wakitoa salamu za rambirambi.

Simu na sms hizo zilimiminika kwenye ofisi ya gazeti hili kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, kudhihirisha namna uvumi huo ulivyopata umaarufu katika kona mbalimbali za nchi.

Uchunguzi uliofanywa na waandishi wetu wikiendi iliyopita umebaini kuwa, Mpakanjia bado yupo hai, ingawa hali yake ni mbaya na amelazwa kwenye Hospitali ya Jeshi, Lugalo, Dar es Salaam.

Uchunguzi huo ulibaini kwamba, mfanyabiasha huyo amelazwa kwenye wadi ya watu maalumu (VIP), lakini anakula na kujisadia haja ndogo kwa msaada wa mipira.

Ijumaa Wikienda linatoa pole kwa familia ya Mohammed Mpanjia kuhusiana na uvumi wa habari hizo za kifo, pia linamuombea afya njema mfanyabiashara huyo ili arejee katika hali nzuri.


BUBU HUYU HAFAI...

Inatoka Uk 1
Bubu huyo ambaye ni mkazi wa Iringa mjini, anamiliki danguro hilo ndani ya moja ya gesti zilizopo kwenye Eneo la Mshindo, mkoani humo.

Vyanzo mbalimbali vya gazeti hili, vilieleza kuwa mbali na kufanya biashara hiyo, pia Shambe huwapigisha picha za utupu warembo anaowamiliki na kuziuza kama mali halali.

Vyanzo hivyo viliongeza kuwa mlemavu huyo huwauza mabinti wa danguro lake kwa gharama tofauti, kulingana na muda ambao mteja atahudumiwa, pia thamani ya picha huendana na ubora pamoja na uzuri wa wapigwaji.

“Kwa mfano, mteja akitaka kulala na mwanamke mmoja kuanzia usiku hadi asubuhi, Bubu huwa anawatoza shilingi 2,500 hadi 3,000, lakini kama atataka huduma ya ‘chapu chapu’ huwa wanamlipa shilingi 1,000 au 1,500,” kilisema moja ya vyanzo vyetu.

Ilielezwa na chanzo kingine kuwa Shambe ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Bubu, mara nyingi huzingatia uzuri na umri wa binti anayemmliki.

“Wale ambao ni wazoefu gharama yake siyo kubwa, lakini mabinti wadogo na wanawake wenye mvuto, mara nyingi bei zao hufikia mpaka shilingi 5,000.

“Hata kwenye picha, kama picha ni nzuri na wanawake ni warembo huziuza kwa shilingi 2,000, kama ubora wake ni mdogo huziuza kwa shilingi 1,500 au 1,000,” kilisema chanzo chetu kingine.

Wiki iliyopita, gazeti hili, lilimtuma mwandishi wetu, Iringa, kwenda kufanya upelelezi kwenye gesti inayodaiwa kutumiwa na Shambe kama danguro.

Katika upelelezi huo, mwandishi wetu alifanikiwa kumpata Shambe ambapo alimlipa shilingi 1,000 na kukabidhiwa mrembo mmoja katika kipindi cha saa mbili.

Aidha, mlemavu huyo alimuuzia mwandishi wetu picha tofauti za utupu ambazo aliwapiga mabinti waliopo kwenye danguro lake na nyingine akiwa amepozi nao.

Katika mahojiano na mwandishi wetu, dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Anitha ambaye ni mmoja wa mabinti waliopo kwenye danguro la Shambe, alisema, wanalazika kufanya kazi hiyo kwa sababu ya ugumu wa maisha.

Anitha aliongeza, yeye kama walivyo wenzake wametokea kwenye vijiji tofauti mkoani Iringa na waliangukia kwenye danguro la Bubu baada ya kukosa uelekeo wa kimaisha mjini.

Alisema, licha ya kwamba Bubu huwa anawalipa vizuri lakini hapendi kujiuza kwakuwa ni hali ya kujidhalilisha.

Ijumaa Wikienda bado lipo kwenye mapambano ya vitendo hatarishi vya gonjwa hatari la ukimwi, hatupendi ndiyo maana tunayaweka wazi kwa jamii ili wanaohusika wafuatilie na adhabu kali ichukuliwe kwa waharibifu.
Mhariri.
(pichazaidi: http://www.globalpublisherstz.com/2007/08/26/meddy_mpakanjia.html)