Saturday, July 25, 2009

DATA ZA MREFU KULIKO HASHIM THABIT HIZI HAPA!




Huyu mchizi anaitwa Baraka Magesa au maarufu kama 'Baraka Tolu' ana umri wa miaka 18 ana urefu wa futi 7.4 akiwa amepita tolu wetu Hashim Thabit ambaye ana futi 7.3. Naye anacheza mpira wa kikapu alikuwepo kwenye maonyesho ya sabasaba akionyesha shoo ya basketball. Na yeye ana ndoto za kwenda kucheza NBA..

Kwa habari zaidi za huyu bingwa link ni hii:NIFAHAMISHE.COM

Hashim Thabit

MREFU KULIKO HASHIM THABIT?

Kama ulifikiri Hashim Thabit ndiye mrefu peke yake Bongo, ulikosea....kuna kijana mwingine ambaye anadhaniwa ni mrefu kuliko hata Hashim..yuko maeneo ya Gongolamboto/Banana jijini Dar es salaam. Juzi kati alilleta kizaa zaa kikubwa pale alipoibuka mitaa ya Aggrey Kariakoo...alikuwa kivutio kwa kila aliyemuona, alifunga mtaa watu wakimshangaa na kumgombania kupiga nae picha..kila aliyetaka kupiga nae picha alitoa Buku..jamaa aliondoka na kama fote hivi! Hapo unapomuona yumo ndani ya saluni moja na alikuwa anakaribia kugusa siling! mpaka sasa hajajulikana jina lake kamili na anafanya nini...tunaendelea kumfuatilia ili kuwaletea data zake kamili, kwani watu wanasema urefu wa jamaa ni DILI!

KAMA ULIFIKIRI NI DAR PEKE YAKE, FIKIRI MARA 2!

Usivunje Mbavu

Jamaa akipata taswira kwa ukaribu zaidi
Big is Beatiful
Jamaa akijikinga na virusi vya kompyuta
jamaa kaamua kutumia marker pen kuipaka rangi gari yake

Picha zaidi unaweza ukawapa wadau link hii
www.nifahamishe.com

Friday, July 24, 2009

ANATESA UINGEREZA!

Anaitwa TOLULA ADEYEMI (24), ni binti wa Kinigeria ambaye kwa sasa anatesa nchini Uingereza kama Model, DJ na Actress! Kipaji chake kilivumbuliwa mtaani tu....!

STAILI MPYA!!!!

Huyu ni mwana dada Rihana akiwa katika staili mpya ya nywele. Hapa alikuwa akihudhuria uzinduzi wa filamu mpya ya QUENTIN TARANTINO mjini London Alhamis usiku...mnaopenda kuiga fasheni kazi kwenu..!!!

First Flapping, Two-Winged Aircraft Takes Flight

July 24, 2009 -- The world's first successful flight of a self-powered, rudderless, flapping aircraft has been achieved by engineers from AeroVironment.

The NAV, or nano air vehicle, operates by using two flapping wings, which also function as the rudder, elevators, ailerons and engine. With its two wings, the NAV is able to hover, move forward and backwards, and change its elevation. In flight, the NAV almost appears to replicate the movements of a hummingbird.

Simplified, most airplanes and helicopters today fly using the same principle: Air rushing over a shaped and immovable wing (or helicopter blade) produces an area of high pressure below the wing and an area of low pressure. The difference pushes the wing up in the direction of low pressure, creating lift.

An airplane is steered using adjustable flaps on the ends of the wings and at the tail, which also help steady the aircraft.

"It's extremely complicated and technically challenging to come up with ways to control an aircraft with two flapping wings,"said Matt Keennon of AeroVironment, "but this is the closest anyone has come to a rudderless, flapping aircraft."

flying car

IJUMAA SHOWBIZ!

Irene Uwoya: Ndoa kwanza, zawadi za Sexiest Girl baadaye
Miss Tanzania namba tano 2006-07, Irene Uwoya Ndikumana hakuweza kuchukua zawadi zake baada ya kuibuka mshindi wa taji la Ijumaa Sexiest Girl 2008-09. Irene a.k.a Shemeji wa Wanyarwanda alipokuwa nchini, mara kwa mara alipanga appointment na mmoja wa waratibu wa shindano hilo lakini mambo hayakuweza kwenda kama inavyotakiwa kwa sababu muda mwingi alikuwa kwenye pilika za ndoa.

Mrembo huyo ambaye hivi sasa ameibukia kuwa muigizaji funika bovu nchini, mpaka anafunga ndoa na kuondoka nchini kuelekea Cyprus bado alikuwa hajakamata stahiki yake ya ushindi wa Ijumaa Sexiest Girl 2008-09 ambayo ni shopping ya nguvu.

Kwa mashabiki wa Ijumaa Sexiest Girl, taratibu za mawasiliano kati ya waratibu na Irene zinaendelea, itakapofikia wakati wa makabidhiano kila kitu kitafanyika katika picha.
******
Hey! Babu hajafulia
Supastaa mwenye ‘eji’ ya kutosha Bongo Flava, Horoun Kahena ‘Inspector’ ameachia dude jipya linalokwenda kwa jina la Sijafulia.

Inspector a.k.a Babu alilonga na Showbiz kwa njia ya waya na kuiambia kuwa sababu ya kuiweka hewani Sijafulia ni kutaka kuwadhihirishia mashabiki wake kwamba mambo yake ni supa.

“Yap watu wanaongea, wengine wanafikiria nimeishiwa lakini mimi nipo mzuka sana. Zaidi ya yote nina familia ambayo inanikip bize,” alisema mfalme huyo wa Rap Katuni.

Apart of that, Babu alisema kuwa hivi sasa yupo chimbo kwenye studio za Bongo Records chini prodyuza, Paul Matthias ‘P. Funky’ akiunda dude lingine ambalo amekamua pamoja na Hamis Mnjuma ‘Mwana FA’.
Hey, si ilielezwa Babu ana bifu na FA? Stay tuned 4 da song!
********

JANET JACKSON KUZIBA MAPENGO YA THE JACKO
Janet Jackson tayari ameshatangaza kwamba atakuwa tayari kuwalea watoto watatu wa marehemu kaka yake, Michael Jackson ‘The Jacko’.

Aliweka wazi kuwa ataambatana na memba waliobaki wa Kundi la Jackson 5 ili kutoa shoo 50 za London, England ambazo zilitakiwa zitekelezwe na King MJ lakini kwa bahati mbaya Mungu akawa amemchukua mapema.

Kutokana na moyo huo wa upendo ambao Janet anauonesha, wadau mbalimbali wamekuwa wakimminia pongezi kwa maelezo kuwa anaonesha mapenzi yake ya wazi kwa kaka yake.

Kutokana na kukubali kwake kushiriki ziara ya London 02, mratibu wa shoo hizo alisema kuwa anaamini kwamba Janet, 43, atafunika vibaya.

Aidha, inaelezwa kwamba watoto wa Michael, Prince I, Paris na Prince II wanamuona Janet ndiyo chaguo lao kwa sababu hawafikirii mtu mwingine anayeweza kuwalea kwa mapenzi makubwa kama shangazi yao huyo.
********
Ijumaa Sexiest Barchelor. whoz next?
Steven Charles Kanumba ‘The Great’ ndiye aliyebeba taji mwaka 2007, alimpiga mweleka Golikipa wa Simba, Juma Kaseja Juma (PICHANI KULIA) ambaye aliambulia nafasi ya pili.
Tangu wakati huo, mambo yalipoa lakini mwaka huu shindano hilo linakuja kivingine, nani ataibuka kidedea? Ni suala la kusubiri muda, everything gona be mwake.

Ni Kanumba tena? Je anaruhusiwa kutetea taji? Piga simu utoe maoni yako kama The Great aendelee kutetea nafasi yake au apumzishwe na asiingie kabisa kwenye shindano.

Tuma sms utaje jina la staa wa kiume unayedhani anatosha kuwa Ijumaa Sexiest Bachelor 2009-2010. Kumbuka Kaseja alifunga ndoa mwaka jana na mtoto wa Kitanga, Nasra Nassor, hivyo haruhusiwi.
********
kazi kwenu ladies, changamkieni mchongo huo!!!

Thursday, July 23, 2009

IT IS ADVISED NOT TO CONSUME RED BULL. IT IS A VERY DANGEROUS DRINK!

As a public health safety, please pass on this email to all the contacts in your address book especially those with teenage children… and make copies to show to all the people you know…

This drink is SOLD in all the supermarkets IN OUR country… and our children ARE CONSUMING IT ON A TRIAL BASIS… IT can be mortal…

RED BULL was created to stimulate the brains in people who are subjected to great physical force and in “stress coma” and never to be consumed like an innocent drink or soda pop. RED BULL IS the energizer DRINK that is commercialized world-wide with its slogan:

'It increases endurance; awakens the concentration capacity and the speed of reaction, offers more energy and improves the mood. All this can be found in a can of RED BULL, the power drink of the millennium.!

'Red Bull has managed to arrive at almost 100 countries worldwide. The RED BULL logo is targeted at young people and sportsmen, two attractive segments that have been captivated by the stimulus that the drink provides.

It was created by Dietrich Mateschitz, an industrialist of Austrian origin who discovered the drink by chance. It happened during a business trip to Hong Kong, when he was working at a factory that manufactured toothbrushes.

The liquid, based on a formula that contained caffeine and taurine, caused a rage in that country. Imagine the grand success of this drink in Europe where the product still did not exist, besides it was a superb opportunity to become an entrepreneur.

BUT THE TRUTH ABOUT THIS DRINK IS ANOTHER THING:
FRANCE and DENMARK have just prohibited it as a cocktail of death, due to its vitamin components mixed with GLUCURONOLACTONE', a highly dangerous chemical, which was developed by the United States Department of Defense during 60 years to stimulate the moral of the troops based in VIETNAM, which acted like a hallucinogenic drug that calmed the stress of the war.

But their effects in the organism were so devastating, that it was discontinued, because of the high index of cases of migraines, cerebral tumors and diseases of the liver that was evident in the soldiers who consumed it.

And in spite of it, in the can of RED BULL you can still find as one of its components: GLUCURONOLACTONE, categorized medically as a stimulant.

But what it does not say on the can of RED BULL, are the consequences of its consumption, and that has forced us to place a series of WARNINGS:

1. It is dangerous to take it if you do not engage in physical exercise afterwards, since its energizing function accelerates the heart rate and can cause a sudden attack.

2. You run the risk of undergoing a cerebral hemorrhage, because RED BULL contains components that dilute the blood so that the heart utilizes less energy to pump the blood, and thus be able to deliver physical force with less effort being exerted.

3. It is prohibited to mix RED BULL with alcohol, because the mixture turns the drink into a “Deadly Bomb” that attacks the liver directly, causing the affected area never to regenerate anymore.

4. One of the main components of RED BULL is the B12 vitamin, used in medicine to recover patients who are in a coma; from here the hypertension and the state of excitement which is experienced after taking it, as if you were in a drunken state.

5. The regular consumption of RED BULL triggers off symptoms in the form of a series of irreversible nervous and neuronal diseases.

CONCLUSION: It is a drink that should be prohibited in the countries of the Caribbean and Latin America, (and the entire world) as it is already waking up other nations because when it is mixed with alcohol it creates a time bomb for the human body, mainly between innocent adolescents and adults with little experience..

LISHE NDIYO KILA KITU KWA MWENYE VIRUSI

You are what you eat
Katika makala zetu zilizopita, tuliwahi kuandika kuhusu dhana nzima ya Ukimwi na kusema kuwa Ukimwi siyo ugonjwa bali ni hali. Tulifafanua kuwa maana ya UKIMWI ni ‘dalili’ ya Upungufu wa Kinga Mwilini na siyo ugonjwa kama baadhi ya watu wanavyodhani.

Aidha, tulisema kuwa, kwa tafsiri hiyo ya UKIMWI, ina maana kwamba kila mwenye UKIMWI siyo lazima ana VIRUSI vinavyosababisha Upungufu wa Kinga Mwilini na kila mwenye VIRUSI (HIV Positive) siyo lazima ana UKIMWI. Hii ni dhana pana ambayo ikieleweka vizuri, umuhimu wa lishe mwilini nao utaeleweka vyema.

Katika mfululizo wa makala haya yatayoanza leo, tutaangalia ni kwa nini lishe ndiyo kila kitu kwa mtu anayeishi na virusi vinavyosababisha UKIMWI. Nimepata maombi mengi kutoka kwa wasomaji wetu wakitaka pia tuwakumbuke wenzetu wanaoishi na virusi vya Ukimwi kwa kuwakumbusha lishe sahaihi itakayowasaidia kuwapa kinga imara dhidi ya maradhi nyemelezi.

Kwa nini lishe bora ni muhimu zaidi kwa wenye virusi?
Lishe bora ni muhimu kwa wenye virusi vya Ukimwi kwa sababu hufanya mfumo wa kinga mwilini kuwa imara, hivyo kuusaida kupambana na maradhi ipasavyo. Pia lishe bora huboresha maisha. Lishe bora ni haki na wajibu wa kila mtu, hata kwa wale ambao hawajaathirika.

Bila lishe bora, matatizo ya kupungua uzito, kwashakoo yataendelea kuwa mambo ya kawaida, licha ya kutumia dawa za kuongeza kinga, na hali hiyo inaweza kuchangia kupatwa na magonjwa mengine hatari. Halikadhalika, lishe bora hufanya dawa unazokula zifanye kazi sawaswa.

Aidha, lishe bora pamoja na mazoezi, huweza kuondoa dalili za magonjwa kama vile kuharisha, kusikia kichefuchefu, kutapika, kusikia uchovu, shinikizo la damu na kisukari.

Hivyo basi, ili mtu mwenye virusi na ukimwi aweze kuendelea kuishi maisha ya afya, ni lazima azingatie lishe hiyo bora. Pengine mtu utajiuliza, lishe bora ni ipi na unawezaje kuijenga? Hapa tunakuelimisha ifutavyo:

LISHE BORA NI IPI?
Lishe bora ni ile inayotokana na vyakula vya mboga mboga, matunda, nafaka halisi na vyakula jamii ya maharage, pamoja na vyakula vya protini vyenye mafuta kidogo. Vyakula tajwa hapo juu vina kiwango kikubwa cha virutubisho na vina mchango mkubwa sana kwenye ustawi wa afya yako kuliko vyakula vitokanavyo na sukari na mafuta pekee.

DONDOO ZA KUJENGA LISHE BORA
Kila siku hakikisha unakula mboga mboga na matunda ya kutosha, kwa nyakati tofauti, kiasi cha milo mitano hadi sita, sawa na vikombe vitatu. Kula mboga na matunda mchanganyiko ya rangi tofauti.

Kwa kuwa vyakula vya wanga (carbohydrates) ndivyo vinahimizwa kuliwa kwa wingi kwa mtu mwenye virusi, vyakula utakavyokula kwa siku, asilimia 50 vitokane na nafaka halisi (ugali wa mahindi yasiyokobolewa, mtama, ngano, uji wa ulezi, n.k).

Kula vyakula vya kuongeza protini mwilini ambavyo havina mafuta mengi, kama vile nyama ya kuku (bila ngozi), samaki, nyama steki isiyo na chembe ya futa (lean-meat) na bidhaa zitokanazo na maziwa yasiyokuwa na mafuta (low fat au fat free milk).

Punguza ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi, vyakula vitamu-vitamu na vinywaji baridi, kama vile soda, kwani vina virutubisho vya kutosha na huchangia kuamsha kiwango cha sukari mwilini.

Kila siku kula vyakula vingi vitokanavyo na mbegu mbegu, kama vile karanga, korosho na vyakula jamii ya maharage, kunde, njegere, n.k.

KWA NINI UNYWE MAZIWA YASIYO NA MAFUTA?
Itaendelea kesho

Tuesday, July 21, 2009

SUALA LA WIZI KATIKA ATM

KISA MKASA.....
Bwana Juma alikopa hela katika benki moja jijini dare s salaam zaidi
ya milioni 10 , moja ya masharti ya mkopo huo ni kwamba lazima pesa
hizo zihifadhiwe katika benki hiyo hiyo , na kweli bwana juma alifanya
kama benki ilivyomtaka afanye baada ya wiki moja bwana juma alienda
katika mashine moja ili atoe pesa kidogo kiasi cha shilingi laki
2 ,siku 4 zilizofuatia akaenda kutoa kiasi kama hicho tena , siku 4
tena zilizofuatia akaenda kuchukuwa pesa kutumia mashine hizo akakuta
pesa zake hakuna katika account yake .

Bwana juma hayuko mwenyewe katika kuuliza uliza kwa wateja wengine nao

wakamwambia pia pesa zao zimepotea katika mazingira ya kutatanisha
wakati wanachukuwa pesa katika mashine za ATM , bwana Juma alivyoenda
kuripoti suala hili katika benki husika akaambiwa kwamba inaonyesha
alichukuwa pesa nyingi zaidi katika mashine hizo za ATM siku hizo za
Jumamosi na Jumapili Jioni.

Kumbuka wizi mkubwa katika mashine za ATM unatokea Jioni haswa siku za

mwisho wa wiki , katika siku hizi pia ni ngumu kuwasiliana moja kwa
moja na benki yako kama tukio hilo limetokea papo kwa papo wataweza
kukuambi uende siku za kazi ,ili waweze kushugulikia vizuri tatizo
lako sio kuibiwa pesa tu hata ukidondosha Kadi yako ya ATM mfano pia
ni ngumu kupata mawasiliano ya moja kwa moja na banki hizi mpaka siku
za kazi .

…………………………………………………………………………….


Ukisoma Gazeti la mwananchi la leo kurasa ya mbele wameonyesha mfano

wa jinsi mashine za ATM zinavyotakiwa kuwa pale mteja anapoenda
kuchukuwa pesa katika mashine hizo na pale ambapo vifaa maalumu ya
kuhifadhi taarifa za mteja vinavyoonekana vikichomekwa katika mashine
hizo za ATM .

Kulingana na Gazeti la mwananchi inawezekana bwana Juma hakupewa

mafunzo ya kuweza kutambua mashine za benki zake za kutolea pesa
zilivyo na kama kuna badiliko lolote limetokea katika mashine hizo
bwana juma hakupewa taarifa na benki husika au pengine yeye binafsi
hakutaka kuuliza , au kudadisi utofauti wa mashine mbali mbali za
ATM .

Naamini benki zote huwa na taarifa zote muhimu kuhusu wateja wao ,

kuanzia picha , namba za simu , anuani za barua pepe na mawasiliano
mengine , chochote kikitokea ndani ya benki basi ni wajibu wa benki
kutoa taarifa kwa wateja wake , mfano kama kuna suala la kufunga vifaa
maalumu katika ATM za benki hizo kunakofanywa na wahalifu hawa kama
benk ingekuwa inajua hivyo ingawataarifu wateja wake pamoja na kuweka
picha za mashine za ATM zilivyo na kama kuna badiliko lolote
wajulishwe .

Sasa je hawa wahalifu wanajuaje mfumo wa ATM ? kwanini mhalifu

anaendakatika mashine ya ATM na kuweka kifaa kiurahisi hivyo bila hata
ya Mlinzi kuwa na mashaka nae ina maana vifaa hivi ni vya kufungwa tu
katika sekunde au dakika kadhaa chache mlinzi anakuwa umbali gani na
mashine hizo za ATM hata asiweze kujua kama kuna kitu kipya
kimefungwa ?

Watu wanaoweza kujua mifumo ya mashine hizi ni Wafanyakazi wa Benki ,

wafanyakazi wa kampuni zinazofanya matengenezo katika benki hizo au
zile zilizofunga mashine hizo na sio zaidi ya hao , mtu kuja kufunga
kifaa au vifaa atakuwa kapata taarifa muhimu kuhusu mashine hizo toka
kwa watu hao hapo juu , katika taarifa za gazeti zinasema watu hao ni
raia wa Bulgaria , Katika mashine hizo lugha zinazotumika ni
Kiingereza Na Kiswahili je sisi tuna uhusiano Gani na Bulgaria ? wao
hizo sio lugha zao kuu inawezekana wanapata maelekezo toka watu wa
ndani kwamba kitu Fulani kina maanisha hivi na vile .

Je benki hizi zinatabia za kufuatilia wateja wao kujua tabia Fulani

Fulani kuhusu wateja hao wakati wanachukuwa pesa , najua nchi kama
Nigeria kuna kampuni zimeajiri watu kwa ajili ya kufuatilia wateja wao
katika sehemu nyingi wanazoshugulika na pesa zao kama chochote
kikitokea inakuwa rahisi kufanya maamuzi kutokana na anavyofuatiliwa
na vijana hao ndani ya benki husika au nje ya benki na kampuni ambazo
ziko huru kiutendaji .

Halafu kuna hili suala la mporomoko wa Uchumi duniani , inawezekana

hii hali imechangia kwa kiasi kikubwa kwa benki nyingi kuingia katika
matatizo na wizi wa pesa za watu ndani ya benki , je inawezekana
kwamba kuna mpango maalumu kati ya baadhi ya wenye benki na pesa
zinazoibiwa yaani watu wanakopeshwa pesa hizo hizo zaidi ya miamoja
ili waweze kutengeneza faida haraka haswa kwenye benki ambazo sio za
nchini ? hili pia linawezekana kufanyike uchunguzi tu kuna benki
zinajaribu kudanganya wateja wake kwa njia hii .

Mwisho , suala hili lipo na linaendelea je raia haswa wateja wa benki

hizi wameandaliwaje kupambana na uhalifu huu ? je wachukuwe pesa zao
zote benki au wafanyaje wamepewa njia gani mbadala za kuweza kupamba
na suala hili ? vyombo vyetu vya usalama navyo vinapambana vipi na
suala hili sio lazima vipewe hints na raia wema vinatakiwa navyo
vijipange sehemu mbali mbali kuweza kufuatilia watu hata kujiingiza
kwa makusudi katika makundi ya uhalifu huu kuweza kuwatambua .
***************
By Yona Maro

Ras Makunja na Ngoma Africa aka FFU katika makamuzi Fest-Africa, Finland


Mwanamziki Ras Makunja aka Bw.Kichwa Ngumu na mzimu wake FFU ,juzi jumamosi walifungua ukurasa mpya katika jukwaa la Fest-Africa,kwani waliweza kuwapa burudani ya aina washabiki wa ufini, wanamziki washambuliaji (FFU) wa safu ya mbele waliweza kuwamdudu washabiki vizuri,Ras Makunja kiwaongoza jukwaani washambuliaji wake wa safu ya mbele mpiga solo Chris-B,ambaye pia anaimba na Bi.Severne aka Sevasha au afande wa kike,huku mdundo mkali wa The Ngoma Africa Band ukiwasindikiza na kuweza kufanikiwa kuwayumbisha washabiki katika onyesho hilo! Kitu cha kufurahisha mziki huo wa Ngoma Africa uliweza kuwazoa washabiki na kupanda jukwaani kusakata ngoma za moto! mojawapo ya walivutwa jukwaa ni "Mzee Mponda" au tumwite "Dady Mponda" alipanda jukwaani na akawashangaza maelfu ya washabiki kuwa "kuwa wazee wa Kiafrika" wanajua kucheza mziki na kutoa ushindani kwa vijana! wasikilize ngoma afrika hapa http://www.myspace.com/thengomaafrica
(imetumwa na mdau mwenyewe)

Monday, July 20, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Bow wow:kumbe dogo amejikunja na mademu sita wakiwemo hawa
Ishu ni malavi davi, yanamhusu kila mtu kwa sababu ndiyo sanaa kiranja katika maisha ya binadamu. Ukisema hayakuhusu that means mambo yako siyo mazuri! Ebwana dah!

Ni dogo aliyekulia kwenye Hip Hop na akaanza kusanya noti akiwa na umri wa primary school kabla ya kuibukia kuwa tajiri wa mfano kwa wajasiriamali wengine.
Ni mapenzi sasa, dogo alitimiza umri wa miaka 18 miaka minne iliyopita na inahisiwa kwamba alianza sanaa ya mapenzi akiwa U-18.

Amekwishatoka na mademu sita ambao wanatambulika, wa kwanza ni Dolicia Bryant baadaye akaanza kumegana kisela na mwanamuziki Ciara mwaka 2005 kabla ya kupigana chini mwaka 2006.

Alipoachana na Ciara, dogo alihamishia jeshi kwa Paula DeAnda mwaka 2007, akazinguana naye na kugeukia kwa Angela Simmons ambaye alijikunja naye from 2007 up to 2008.

Kipindi akiwa na Angela Simmons, ‘bwa mdogo’ alionesha ujuzi kwa kucheza nje-cup na mwanadada Melody Thormon kwa maana hiyo in a same year, aliwatumia watatu ukimuongeza na Paula DeAnda. Hata hivyo, tangu mwaka jana (2008) dogo amejituliza kwa mrembo Karrine Steffans.

Jina lake kamili ni Shad Gregory Moss, alizaliwa Reynoldsburg, OH, Marekani Machi 9, 1987. A.K.A zake nyingine ni bow weezy,
bow wizzle na hapa juzi kati alitangaza kusain out katika game ya Hip Hop kwa maelezo kwamba kila kitu alichokihitaji anacho.

Pesa anazo, umaarufu anao wa kutosha! Dogo matata eeh! Msomaji kama unapenda kufahamu usiano wa zamai na sasa wa staa yeyote wa kiwanja tuandikie ujumbe mfupi(SMS) ukilitaja jina la muhusika kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173, e-mail:mcgeorge2008@gmail.com. Pamoja sana.

**************************************
MB Dog
Nembo ya wanamuziki wenye sauti za hamasa nchini, Mohamed Mbwana ‘MB Dog’ amefiwa na mwanaye wa kike, Suhaila Mohamed aliyekuwa na umri wa miaka saba.
Suhaila alifariki dunia last weekend, usiku wa kuamkia Jumamosi nyumbani kwa staa huyo Mabibo, Dar es Salaam baada ya kuzidiwa na shambulio kali la malaria.

Insider wetu alitupasha kwamba kabla ya kifo hicho, Suhaila alikuwa arrested by malaria 4 almost mwezi mmoja na kwamba alilazwa Amana Hospital kwa wiki tatu kisha aliruhusiwa kurudi nyumbani ambako alimudu ku-survive kwa wiki moja tu kabla hajaitikia wito wa Mungu.

Mpendwa wetu Suhaila, alizikwa kwenye makaburi ya Mabibo Hostel, Dar juzi (Jumamosi). Hili ni pigo kubwa kwa mwanetu MB, sisi Abby Cool & MC George over the weekend kwa niaba ya readers wetu, tunatoa pole nyingi kwake. Mungu amempenda zaidi.
********************************************

Hizi ni hasira za fans wa...hip hop
Tulistop kuendelea na debate yetu kuhusu Hip Hop kutokana na kifo cha Mfalme wa Pop duniani, Michael Jackson ‘King MJ’ ambaye ali-pass away Juni 25, 2009 Los Angeles, Marekani.
Tutazidi kumkumbuka mtu mzima MJ, alifanya mengi kwenye muziki ndiyo maana pamoja na mambo kibao yaliyokuwa yakizungumzwa kuhusiana naye enzi ya uhai wake lakini inapozungumziwa kazi yake kila mtu anapiga saluti!

That’s for Michael! Baada ya makala yaliyopita kuhusiana na Hip Hop, wadau wengi walituma sms wakichangia yale waliyonayo. Cheki wanavyomwagika;

Easy E aliweka Cul kichwani nae sio mwana HIP HOP na alipenda sana mademu, Ice T aliweka rolers kichwani nae siyo mwana Hip Hop.

**********************
HIP HOP inazidi kufifia au kufa, Bongo wengi imani zao haba, hawajui Hip hop ni nini? Hip Hop haiuzi wala hailipi, pia katika Radio stations, Hip hop haipigwi sana kama R&B na nyinginezo. Kila time ni mapenzi tu.
I am MC Luggy, from Geness High School, Makambako. napenda sana Hip Hop kwa sababu ina ujumbe.
***********************
Hey man, siwafagilii artists wanaojifanya wafuasi, wanaleta makuzi instead of playn their parts! Nimeipenda topic! It’s me Shady!
*********************
Hey ebwana dah! Mc George na Abby Cool sina cha kuongea but i’m waiting mnachokuja nacho katika safu yenu ya Ze real kuhusu Hip Hop! Ni kweli Hip Hop ni harakati siyo watoto wa mama wana wave kichwani! Wanauza sura then wanajita wana-Hip hop.
Barks hapa niko pande za Mbeya City
********************
Wengime wanachana Hip Hop kwa kuwa sauti zao hazina mvuto kwenye R&B. HIP HOP ina nguzo tano baab! Nawashauri wana-Hip Hop wazidumishe ili Watizedi waache msemo kwamba Hip Hop ya ukweli ipo America.
Mussa Kibiki wa Mafinga Iringa.

Hayo ndiyo baadhi ya maoni ya wafuasi wa game ya muziki wa Hip Hop. Cheki na sisi wiki ijayo ili ufahamu tutashuka na ishu gani nyingine.
*************************

Fid Q Yupo next door na fans wake
Staa wa Hip Hop mwenye vocal yenye ujazo mkubwa, Fareed Kubanda ‘Fid Q’ amesema kuwa ameamua kujiweka karibu na fans wake ili kuboresha utendaji kazi wake kimuziki.

Fid Q ambaye anatambaa na a.k.a kibao kama vile Ngosha the Don, Jeshi la Mtu Mmoja alisema kuwa katika mpango huo wa kuwa next door na fans wake, ameanzisha kona ya kuwasiliana nao kwa njia ya sms.

“Hiyo ni fan base yangu, kujiunga unatuma sms yenye neno FIDQ kisha unaituma kwenda nambari 15522,” alisema Ngosha the Don na kujazia: “Huduma hii ni kwa wateja wa mitandao ya simu za mkononi nchini, Tigo, Zain na Vodacom pekee.”
**************************************

Eti Michael Jackson hakuwa rijali!!!
Shoga ambaye pia alikuwa mpenzi wa Daktari wa ngozi wa marehemu Michael Jackson, Arnold Klein ameibuka na kudai kuwa, nyota huyo eti hakuwa rijali kwasababu alikuwa hana uwezo wa kupata watoto.

Katika mahojiano na tovuti moja ya Marekani, shoga huyo, Paul Gohranson alisema kuwa, ‘MJ’ (Michael Jackson) alipoteza uwezo wa kuzalisha mbegu za kiume baada ya siku moja baba yake kumpiga teke la kwenye korodani.

Gohranson aliendelea kudai kuwa, hali hiyo ilisababisha marehemu amuombe daktari wake (wakati huo) Dk Arnold Klein amchangie mbegu zake za kiume ili aweze kupata watoto na kuwa baba.

“Nilimuuliza Arnold kwanini Michael Jackson hatumii mbegu zake za kiume, akanijibu kuwa, (Michael) alikuwa hana uwezo wa kupata mtoto, “ alisema Gohranson.

“Arnold alinielezea matukio mawili ambayo baba yake alimpiga kwenye sehemu zake nyeti.”

Akaongeza: “Katika tukio la kwanza, wakati Michael alipokuwa mdogo, baba yake alimnyanyua kwa mguu mmoja na kuanza kumpiga.”

“Dr Klein alisema kuwa, MJ alimwambia kwamba wakati huo baba yake hakudhamiria kumpiga sehemu zake za siri, lakini alipompiga alisikia maumivu sana.
“MJ alianza kulia wakati baba yake alipozidi kumsema huku akiziminya korodani zake kwa nguvu.”
********************************
compiled by mc george

Sunday, July 19, 2009

MAISHA BILA UKIMWI YANAWEZEKANA

Sio kila muathirika wa UKIMWI ni mzinzi , muhini au alipata ugonjwa huo kwa njia ya ngono au njia zingine zinazohusiana na zinaa au uzinzi , sio kwamba kila mgonjwa wa ukimwi ametaka kupata ugonjwa huu au alitegemea kupata ugonjwa huu , Lakini ni ukweli usiofichika kwamba wengi wa waathirika walijua au walikuwa na uelewa kidogo wa janga lili na mengine yanayoendelea .


HADITHI FUPI
Jana usiku nilitembelea bar moja mwananyamala inaitwa MK , nilikaa chini karibu na kituo cha basi nikawa namsubiri rafiki yangu Fulani , pembeni yangu alikuwa dada mmoja mrefu amekaa na mwanaume mmoja , wanakunywa wanapigana mabusu na kadhalika

Yule msichana akatoka pale kwenda juu , na mimi nilitoka kwenda msalani ufika huko juu nikakuta yule msichana ameingia choo cha wanaume na mwanaume mwingine wanafanya ngono ya chap chap huku yule mwanaume mwingine ameachwa chini pale na bia yake kaambiwa amekuja msalani .

Nilipotoka pale nikakutana na rafiki yangu mwingine hapo hapo juu , ghafla yule msichana akaitwa na mwanaume mwingine kule kule juu , akakaa nae akaagiza kinywaji kisha akamwambia yule mwanaume kwamba amepata simu ya dharura anarudi nyumbani kwake kidogo atarudi

Kumbe harudi nyumbani anarudi chini kwa yule kidume wake aliyemwacha pale , akaa kidogo pale akavamia jukwaa la kusakata rhumba akaanza kusakata rhumba pale na vijana wenzake huku maisha yanaendelea wakaanza kupenda namba za simu pale pale .

Sikujua kama wale wavulana wanajuana au hawajuani au yule msichana ni changudoa anajiuza au hajiuzi lakini alichokuwa anafanya hakikubaliki hata kidogo na kuvunja maadili kwa kiasi kikubwa .

MAISHA YA NGONO
Kijana mdogo yuko zake secondary labda form 2 hivi , anaanza mahusiano ya kimapenzi na mtu , akifika form 4 labda yuko na mpenzi mwingine halafu tuseme huyu kijana sio mwaminifu kwa mpenzi wake ni mtu mwenye tamaa za kimaisha na kadhalika , akimaliza form 4 anaenda A Level ambako anakuwa mbali na mpenzi wake huko alipo anapata mpenzi mwingine , kama ni sehemu mbali sana hawezi kuwasiliana na wazazi wake kama anashida mbali mbali , basi anaweza kupata wapenzi wengine wa kusaidia mambo yake ya kimaisha na kimasomo .

Huyu kijana wakati wa likizo anarudi nyumbani anakutana na yule mpenzi wake wa nyumbani wanafanya mapenzi na kufurahia maisha yao ya mapenzi , kijana kamaliza ALEVEL anaingia chuoni huko nako anakutana na changamoto kibao za kimaisha na anakutana na vishawishi kibao na anakubaliana na vishawishi hivyo anaingia mtegoni napo anafanya mapenzi na anasa zingine .

Akimaliza chuo anatafuta kazi , mtu aliyempatia kazi alimwomba rushwa ya ngono anatoa ngono , kule kazini kidogo anakuwa na uhusiano wa kimapenzi na bosi wake au wafanyakazi wenzake mbali mbali , bado mpenzi wake anaye .

Kijana huyu anaamua kuingia katika ndoa , wanaishi lakini ghafla wanaaanza kumuumwa na kusumbuliwa na maradhi , kupimwa wanakutwa na UKIMWI , sasa kivumbi kinaanza kumtafuta mchawi ni nani .

Kama unavyoona hapo kijana ameanza mapenzi siku nyingi sana na amekuwa na wapenzi mbali mbali wakati wote huo alikuwa hapimi kuangalia afya yake mpaka alipoingia katika ndoa ndio anapima kujua afya yake tena baada ya kuonekana afya yake iko shakani

Kwahiyo vijana wengi na watu wengi wanaishi na virusi kwa zaidi ya miaka 10 au 5 bila wao kujitambua kama wanaukimwi na kama afya zao ziko salama ili waweze kupanga maisha yao mazuri ya mbeleni , hali inazidi kutisha sana .


KUANGALIA AFYA
Wengi hatuna mazoea ya kupima afya zetu kwa ujumla , mfano mimi nina ratiba ya kuangalia afya yangu kila miezi 2 , hiyo imeshawekwa katika ratiba yangu ya maisha yangu siku zote , kwa jumla ya miaka zaidi ya 10 mfululizo sijawahi kusumbuliwa na ugonjwa wowote zaidi ya mafua ambao ni ugonjwa wangu sugu vyengine siumwi .

Kijana yuko katika mahusiano na mtu hataki kujua afya ya mwenzake , sasa najiuliza kama wanapenda kuishi wote kwa miaka 30 ijayo kwanini usijue afya ya mwenzako kwa faida zako wewe ? siku yoyote anaweza kusumbuliwa na hiyo afya yake kama humjui au kama ulikuwa hauna taarifa si ndio unaanza kuona mzigo kumbeba mwenzako na ndio mnakimbiana ?

Kupima afya iwe ni wajibu wa kila mtu haswa vijana ambao taifa linawategemea kwa ajili ya shuguli zaidi sasa hivi na hata siku zijazo , kama vijana hawataki kupima afya zao , taifa haliwezi kujua na halitamudu kuwahudumia vijana wote walioadhirika kwa sababu ya takwimu ndogo au za uwongo walizokuwa nazo .

UKIMWI SIO MWISHO WA MAISHA
Kama unaenda kupima ukajua umeathirika ongea na mpenzi wako nae ajue kuhusu kilichokusimu , uwe wazi kwa mpenzi wako kuhusu mambo haya , wengi hawataki kusema na badala yake wanavunja ndoa au mahusiano na kwenda kuanza maisha mengine na wapenzi au wanandoa wapya

Wengine wanafikia hata hatua ya kwenda makanisani kubadilisha dhehebu na kuokoka , nimeona makanisa mengi ya kilokole siku hizi yamevamiwa na watu waliokata tamaa wameathirika wanaenda kutumia kioo cha ulokole kujisafisha huku wanaendelea na dhambi zao kwa kasi ile ile

Niliwahi kwenda katika msiba mmoja , huyu kijana alikuwa mwathirika , alipoona anakaribia kufa akaamua kwenda kuokoka na kufuta uvumi mitaani kwamba jamaa alikuwa yuko safarini na alikuwa mbeba silaha za maangamizi , kweli mchungaji akampokea yeye mchungaji si anataka sadaka tu ? hataki zaidi ukitoa sadaka wanafanya sala na kukupa huduma zote

Huyu kijana akafariki baada ya wiki 3 hivi , katika mazishi yake mchungaji akamsifia kijana yule kwamba alikuwa kijana mwerevu , mfanyakazi hodari na msikivu , lakini mungu amemchukuwa ghafla kwa ugonjwa wa malaria tunasikitika sana lakini nasi tunaenda huko huko , wote tutaitwa na muumba kwenda kwa njia kama ile tuliyojia nayo

Mchungaji akamaliza kwa hutuba yake , na hapo vijana waliokuwa pembeni wanasikiliza wakaingiwa na ushawishi kwa kwenda nao kujificha makanisani walivyojua wameadhirika , na ni kweli makanisani siku hizi wamejaa wazinzi , waasherati kuliko kipindi chochote cha maisha watu wanatumia makanisa na ulokole wao kuuhadaa ulimwengu .

MSIMAMO WA MAISHA
Wakati Fulani nikiwa secondary mwalimu wangu alifundisha somo Fulani la kujitambua , anasema kijana lazima ujue kwanini umezaliwa , kwanini uko hapo ulipo sasa hivi , unatakiwa ufanye nini kwa maisha yako na wengine wanaokuzunguka na mwisho wa siku ufanye nini kuwa na msingi bora wa maisha yako ya mbeleni .

Kama hauna msimamo wa kujua wewe ni nani na majukumu yako katika dunia hii , pia huwezi kuwa na msimamo wa maisha ya kimapenzi na uhusiano na mpenzi wako , katika kutumia kinga au zana wakati wa kufanya vitendo vya ndoa incase ukitakiwa kufanya hivyo .

Kuna tatizo lingine la vijana wengi kutokuwa na msimamo kuhusu maisha yao yote kuanzia ya kimapenzi na mambo mengine , katika hili siwezi kumshambulia kijana peke yake , tuangalie wazazi wao wanafanya nini au walifanya nini kuhakikisha kijana wao anakuwa mtu mwema na kumweka katika maadili yanayofaa ili kukabiliana na maisha huko mbeleni anapoenda .

Baba yetu alikuwa na mazoea ya kutuita mimi na ndugu zangu wengine kuongea na sisi kila baada ya mwezi mmoja , kuuliza unafanya nini , una mipango gani na kama umeshindwa kitu ni kitu gani umeshindwa , na je kama unataka msaada kutoka kwake wa aina yoyote ile .

Baba yangu ni kati ya wazazi wachache wanaojali sana familia yake na watu wake wa karibu katika mambo yake popote anapoenda na kutembelea , wazazi wengi wanatakiwa wawajengee watoto wao uwezo wa kuwa wawekezaji wazuri na wazalishaji wazuri katika stali zao za maisha .

Kama mtu ukilelewa vyema ukawa na msimamo wake wa maisha hautaweza kuhujumiwa katika mambo mengi tu hapa duniani moja wapo ni hilo la vishawishi vya anasa mbali mbali katika maeneo unayotembelea .

CHANGAMOTO KWA VIJANA
Tunajua kwamba ukimwi upo na utaendea kuwepo hatuna budi kuwa na misimamo yetu haswa ya kujua afya zetu kwa njia ya kupiima ili tuweze kuwa wema na wenye malengo na maisha yetu ya baadaye , ukishapima na kujua majibu yako lazima utakuwa na msimamo Fulani katika maisha yako , lazima utakuwa na mabadiliko Fulani katika maisha na mwenendo wako

Lakini mwisho wa siku suala la ukimwi ni binafsi sana , huwezi kwenda kuongea na kumuelimisha mtu kuhusu UKIMWI kama yeye mwenyewe hajaamua kujielewa na kujitambua majukumu yake katika jamii inayomzunguka .

Nawapa pole wale wote waliadhirika na ugonjwa huu popote walipo lakini wawe na matumaini na maisha mema hapo mbeleni , siwezi kuwalaumu au kuwaponda sio wote wamepata ukimwi kwa kujitakia , wengine wameambukizwa na wapenzi wao wasio waaminifu , wengine bahati mbaya mahospitalini au katika ajali zingine makazini au sehemu wanazotembelea

Wengine ni kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu ugonjwa huu , wengine ni misimamo yao haswa waliokuwa katika mahusiano hata ya ndoa na wengine ni wenyewe wameamua kujitoa mhanga kutokana na maisha kuwabana au kusumbuliwa na msongo wa mawazo

By Yona Fares Maro
I.T. Specialist and Digital Security Consultant