Wednesday, August 15, 2007

CHINJACHINJA


Na Richard Manyota
Mapambano makali kati ya Wananchi wenye hasira na majambazi yaliibuka hivi karibuni eneo la Tabata Matumbi, jijini Dar es Salaam, kiasi cha kuufanya usiku wa manane wa Agosti 10 mwaka huu kuwa wa chinja nikuchinje.

Tukio hilo la aina yake lilitokea baada ya wakazi wa eneo hilo kuchoshwa na oparesheni ya wizi na ujambazi iliyokuwa imetangazwa na kundi la vijana wasiojulikana.

Wakazi wa eneo hilo kwa nyakati tofauti waliliambia gazeti hili ambalo nalo lilituma kamera yake eneo la tukio kuwa, siku za hivi karibuni wananchi wa Tabata walikuwa wakiishi maisha ya hofu kufuatia matukio ya wizi na ujambazi.

Walisema baada ya kuchoshwa na vitendo hivyo, waliamua kukutana ili kujadili njia ya kukomesha wizi na ujambazi ambapo walikubaliana kuendesha msako mkali ulioambatana na ulinzi wa doria ya usiku.

“Baada ya kuona maisha yetu yako hatarini tuliamua kuwasaka wezi hawa, maana ilikuwa haipiti siku bila kusikia mtu kaibiwa, tulianza doria ya kulinda mitaa yetu hasa usiku wa manane.

“Leo hii tukiwa kwenye lindo zetu kundi la hao vijana wakiwa na zana za kukatia nyavu, kuvulia simu dirishani na silaha kadhaa kama mapanga na nondo tuliwabamba, tulipowasimamisha walianza kutushambulia, nasi tukaanza kupamabana nao.

“Tuliwashinda nguvu, wengine walikimbia hawa wawili tuliwanasa wakiwa na zana hizi, wananchi walipokuja wakaanza kuwapiga,” alisema Saidi Amir mkazi wa eneo hilo huku akimwonesha mwandishi zana na majambazi hayo yakiwa hoi.

Aidha katika harakati za kuwanasa wengine zaidi mitaa ya eneo hilo ilifungwa na mayowe kutawala eneo la tukio huku taarifa za wahalifu hao zilipelekwa kituo cha polisi kupitia namba ya dharura ya 112 ambapo msaada wa askari ulitolewa.

Katika hali iliyoonekana kuwa kundi hilo la wezi lilikuwa limeamua kufanya uhalifu baadhi ya watuhumiwa hao walikuwa wamevaa nguo za kininja na magauni yaliyodaiwa kutumika kuwahadaa watu na kuficha silaha za kutumia katika ujambazi wao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Masindoki Masindoki alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo aliwasifu wananchi wa eneo hilo kwa ushirikiano wao na kuongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea.


MTOTO ABAKWA

Na Waandishi Wetu.
Mtoto wa kike mwenye umri wa mika 17 anadaiwa kubakwa mara kadhaa na kijana Jabir Said mkazi wa Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam, na kupewa ujauzito.

Imedaiwa na chanzo chetu cha habari kuwa, binti huyo mdogo ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili (jina lake na shule yake linahifadhiwa kwa sababu za kimaadili) alirubuniwa kimapenzi na kijana huyo kiasi cha kushindwa kuhudhuria vyema masomo yake.

Kufuatia vitendo vya ubakaji wa mara kwa mara alivyokuwa akifanyiwa mtoto huyo, wasamaria wema walitoa taarifa hizo kituo cha polisi na kwa waandishi wa habari hizi ambapo mtego wa kuwanasa uliandaliwa.

Mwishoni mwa wiki iliyopita kijana huyo akiwa na binti huyo chumbani wakidaiwa kufanya mapenzi, walifumwa na askari polisi wa kituo cha Magomeni ambapo mtuhumiwa alitiwa mbaroni.

Mmoja wa wasamaria wema ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alisema kuwa, wao kama wazazi na walezi hawakupendezwa na kitendo cha kijana huyo kumdanganya mwanafunzi ndiyo maana waliamua kutoa taarifa hizo polisi.

"Yaani nashangaa sisi wazazi tunajinyima ili watoto wetu wasome matokeo yake wanaishia kwa wanaume, hapana tuliona ni vema hatua zikachukuliwa ili liwe fundisho,” alisema msamaria huyo.

Katika hali nyingine ambayo Amani ilipata taarifa zake ni kwamba binti huyo mdogo baada ya kupelekwa kituoni hapo na baadaye kupelekwa hospitali kupimwa iligundulika kuwa, tayari alikuwa na ujauzito wa miezi miwili.

Naye Baba mlezi wa mwanafunzi huyo Bw.Mrisho Swedi akiongea na waandishi wetu alisema kwamba alikuwa akimuonya mara kwa mara binti yake huyo azingatie masomo na aachane na tabia mbaya lakini hakumsikia.

“Walimu wake walikuwa wakiniambia kuwa mahudhurio yake sio mazuri na kila siku walikuwa wakitoka shuleni saa 8.30 mchana, lakini alikuwa akifika nyumbani kuanzia saa 12 hadi saa 1 usiku, nikimuuliza ananijibu alikuwa tuisheni,” alisema Bw.Mrisho kwa masikitiko.

Gazeti hili linalaani vitendo vya ubakaji vinavyofanywa na baadhi ya wanaume, hasa kwa watoto wadogo ambao mara nyingi wamekuwa wakiumizwa na kuambukizwa magonjwa ya zinaa zikiwemo mimba za utotoni.

Big Brother Africa II

'Housemates' wakwanza kukisi jumbani.. Meryl (Namibia) na Kwaku (Ghana) (sorry for the mistake)
Wengine ni kicheko tu...
'nakumbuka nyumbani jamani..!' Mtanzania Richard ndani ya BBA house

Hammy Jei hoi!


Na Issa Mnally
Dereva teksi wa Kinondoni, Mkwajuni jijini Dar es Salaam aliyefahamika kwa jina moja la Njaidi, a.k.a Hammy Jey, mwishoni mwa wiki iliyopita alijikuta akiwa hoi bin taaban kutokana na umbo lake kuwa kubwa na wingi wa pombe aliyokunywa iliyomfanya aheme kwa shida alipokuwa akicheza muziki.

Tukio hilo la aina yake lilitokea katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini wakati Bendi ya African Stars, Twanga Pepeta ilipokuwa ikifanya onyesho lake.

Dareva huyo wa teksi ambaye mashabiki wa muziki walimpachika jina la Hammy Jei kutokana na vituko alivyokuwa akivifanya, alivamia jukwaa baada ya kuitwa na mwanamuziki wa bendi hiyo, Luiza Mbutu aonyeshe manjonjo.

"Sasa namuita kibonge Njaidi , aje mbele awaoyeshe mashabiki namna ya kucheza mugongo mugongo kwa wanaume wenye vitambi," alisema Mbutu kabla shabiki huyo ambaye mashabiki walikuwa wakimwita kwa jina la Msanii wa Kundi la Ze Comedy, Lucas Mhuvile, Joti au Hammy Jei.

Huku akiwa ameonekana 'kuutwika mtungi' kisawasawa, Hammy Jei alichomoka sehemu aliyokaa na kupanda jukwaani kisha kuanza kunengua kwa staili mbali mbali na kuwaacha hoi kwa kicheko mashabiki wa bendi hiyo pale alipoamua kulaala chali huku akiigiza kuongea na simu.

Ukumbi mzima ulirindima kwa mayowe na vifijo baada ya dereva huyo kuonyesha umahiri wa kunengua kwa kutumia mgongo na wakati mwingine tumbo lake kubwa.

Baada ya kuwafurahisha watu waliokuwemo ukumbini hapo kwa burudani yake, Hammy Jei alionekana akiwa hoi kwa uchovu, lakini hata hivyo aliondoka na kitita!


Miss Mzizima afanyiwa kitu mbaya

Issa Mnally na Imelda Mtema
Aliyewahi kushiriki mashindano ya kumsaka mrembo wa Tanzania mwaka juzi na Miss Mzizima namba 2 wa mwaka huo, Jacqueline Patric, amefanyiwa kitu mbaya na mama mwenye nyumba wake kufuatia ugomvi mkubwa ulioibuka baina yao.

Tukio hilo lilitokea Agosti 12, mwaka huu saa 9 alasiri, Mikocheni, jijini Dar es Salaam.

Akiongea na mwandishi wetu kwa simu, jirani wa mrembo huyo ambaye hakupenda kutaja jina lake, alisema kuwa chanzo cha ugomvi huo ni kitendo cha mama mwenye nyumba wake kumtaka ahame ifikapo mwisho wa mwezi Septemba mwaka huu.

Habari zaidi zinasema kuwa tangu amtake kuhama kumetokea hali ya kutoelewana baina yao.

Akielezea zaidi kuhusu tukio hilo, jirani huyo alisema kuwa Jack aliegesha gari lake vibaya na kuziba njia inayopita karibu na nyumba anayoishi.

Kufuatia hali hiyo, habari zinasema kuwa, wapita njia walilalamikia kitendo hicho lakini mrembo huyo hakutaka kuliondoa.

Habari zaidi zinasema kuwa baada ya mrembo huyo kugoma kuliondoa, mama mwenye nyumba wake aliyefahamika kwa jina la Felicia Ndimbo aliingilia kati na kumtaka aliondoe.

"Mama huyo alimwambia Jack aondoe gari hilo lakini mrembo huyo hakukubali na kuanza kumtolea maneno ya kashfa," kilisema chanzo hicho cha habari.

Tukio hilo lilikuwa kama sinema au 'muvi' ya bure, kwani watu walioshuhudia walikuwa wakicheka jinsi wawili hao walivyokuwa wakipeana maneno mazito ya kashfa.

Habari zaidi zinasema kuwa wawili hao walianza kutupiana matusi na ndipo wakashikana na kupeana mkong'oto wa kutosha ambapo Felicia alikimbilia polisi na kuwataarifu kuwa kafanyiwa fujo na mrembo huyo.

Polisi walikwenda na kumkamata Jack ambapo alitupwa rumande na kufungulia jalada OB/RB/13654/07 shambulio la kudhuru mwili.
Hadi tunakwenda mitamboni, mrembo huyo alikuwa akiendelea kusota rumande.

Tuesday, August 14, 2007

EDITOR WA RISASI AJIBU

DEAR CHAHALI,

Tumefuatilia critisism zako na maoni ya wachangajiaji waliokuwa wakifuatilia mjadala wa habari ya Risasi uliyoishutumu kuwa ina ujanja ujanja ndani yake, kwa takribani siku saba na leo tunaamua kuhitimisha kwa kusema mambo mawili makubwa yafuatayo:-

1: Hatukukurupuka kuchapisha habari ile wala hatukuwa na nia ya ‘kuwadanganya wasomaji wetu’ (deceiving our readers, as you put it) kwani tulipewa ‘tip’ na msomaji wetu ambayo tulifuatilia na kukuta profile za akina dada watatu akiwemo huyo dada aliyejiita Melanie ambaye alijitambulisha kuwa ni Mtanzania anayefanya kazi katika miji ya Miami na Dar es Salaam.

Hivyo hoja hapa ingekuwa ‘tumedanganywa’ na huyo mtoa habari wetu na huyo dada aliyeamua kutumia picha ya mtu mwingine (kama ni kweli), kwani hii si mara ya kwanza kukuta picha za watanzania kwenye mtandao wa Hi 5 na kuziandika (rejea stori na picha ya Mtangazaji mmoja wa Redio Clouds) ambazo ni ya kweli.

Kwetu sisi isingekuwa stori kama tungejua picha zile ni za Mmarekani, kwani stori hapo ilikuwa ni kukuta jina la Mtanzania akiwa amepiga picha ambazo kwa mila na utamaduni wetu bado ni kitu kigeni ambacho kinalaaniwa.

Na kama Bw. Chahali ulisoma vizuri ‘profile’ ya huyo binti utabaini kuwa, kuna sehemu anaeleza bayana nia yake ya kumnasa mwanamuziki wa hapa nchini Rehema Chalamila ‘Ray C’ anayesifika kwa kujua kutumia kiuno chake awapo jukwaani.

Pia kuonekana Miami ni jambo ambalo hata kwenye profile yake ndivyo alivyosema na Mtanzania kuwa Porn Star Marekani haliwezi kuwa jambo geni ikiwa tayari tunao warembo wa fani tofauti ambao ni watanzania wanaoishi huko na baadhi yao wanajihusisha na vitendo vya kifuska.

2: Bw. Chahali unadai kuwa sisi ni waumini wa msemo “offence is the best form of defence” (matusi ndo njia bora ya kujilinda) kwa kuwa hoja zetu tulizozitoa tangu tuisome makala yako zimekuwa zikiegemea kujadili upeo wako wa kupambanua mambo pamoja na elimu yako, tunasema hilo kwa kuwa ulianza mwenyewe!

Kimsingi tunaamini kuwa mtu aliyesoma, akawa na tabia ya kujisomea na kuongeza maarifa kichwani mwake hufanikiwa maishani, lakini yule anayependa kutumia masikio zaidi kupata taarifa kuna uwezekano mkubwa akakosa taarifa sahihi katika wakati sahihi hivyo hujikuta anakosa maarifa.

Aidha, tunaamini mtu anayesoma vitabu huongeza maarifa, akili na hupanua uelewa wake katika mambo ya dunia. Hivyo, ni ukweli ulio wazi kuwa watu wanaopenda kusoma sana vitabu au waliosoma sana wana uwezo mkubwa wa kuchambua mambo kuliko watu wasiopenda kusoma!

Elimu humsaidia mwanadamu kupanua uwezo wa kufanya maamuzi sahihi. Hivyo tulilazimika kujenga hoja zetu kwa kuchambua uwezo wako kwa kuwa katika makala yako ulionesha kujenga hoja kwa misingi ya dharau na kebehi huku ukionesha kutokuwa tayari kufungua milango ya taarifa kuingia kwenye ubongo wako.

Katika dunia tunayoishi, ambayo sayansi na tekinologia inakua kwa kasi, kuna vyanzo vingi vya habari, hivyo kutegemea masikio peke yake kuweza kupata habari ni sawa na kuachwa na wakati, nasi hatuko tayari kwa hilo, tunahitaji kusonga mbele ndio maana tunafanya kila tunaloweza kwenda sambamba na kasi ya dunia kwa kutumia vema vyanzo vyote vya habari (hiki ndicho tulichokifanya katika habari ile inayotuhumiwa).

Mwisho, Chahali tunashukuru kwa chang’amoto uliyotupatia na bila shaka umetujua ni watu wa aina gani. Sisi si watu tusiotaka kujifunza vitu vipya na kujifanya tunajua kila kitu. Hivyo tutafanyia kazi yakinifu mambo yote yaliyochangiwa katika mjadala wote unaoihusu habari ile ili tusije achwa na wakati.

Tunawaheshimu watanzania na kamwe hatutawapa taarifa potofu katika misingi ya kutaka kupata faida na tunapokosolewa, heshima iwekwe mbele!

Asanteni kwa kunisoma,
Sub-Editor, Risasi Newspaper,
Tulizo Kilaga
+255 0715 888887

CHAHALI, NAHITIMISHA MJADALA!

This summary is not available. Please click here to view the post.

TUKO MSTARI WA MBELE KUSAIDIA JAMII, HATUNA TAMAA YA PESA!

Hivi ndivyo alivyokuwa akiishi binti huyu, alisumbuliwa na ugonjwa wa moyo kwa muda mrefu, lakini baada ya kuonwa na Uwazi, tuliandika habari zake na kuhimiza Watanzania kumsaidia na hatimaye kufanikiwa kupelekwa India alikofanyiwa oparesheni iliyobadili maisha yake kupitia Global Publishers!
Baada ya matatizo ya miAka kadhaa aliyoyapata kabla ya kuonwa na Global Publishers, hatimae binti huyu maarufu sasa, Ngendelaki Idd, anaishi maisha ya furaha akiwa ameolewa na ana watoto, katika watu ambao kamwe hawataisahau Global Publishers katika maisha yao, ni pamoja na huyu. WE CHANGE PEOPLE'S LIVES!

Kabla ya kuonwa na kamera za Global Publishers, hali yake ilikuwa hivi binadamu huyu!
Baada ya kufanyiwa operesheni na kurudi katika hali yake ya kawaida kwa gharama za Global Publishers.
Kabla ya kufanyiwa oparesheni, suruali kwake ilikuwa ni 'luxury'
Baada ya kufanyiwa opareshini na kuweza kuvaa 'mkanda nje' tena
Alivyokuwa kabla ya kufanyiwa oparesheni
Alivyo sasa baada ya kufanyiwa opareshini katika hospitali ya Dr. Mvungi Kinondoni jijini Dar kwa gharama za Global Publishers, kupitia kitengo chake cha Community Project.

MWONGOZO BORA WA ULAJI - 2


Wiki iliyopita tulianza sehemu ya kwanza ya makala haya na tuliangalia miongozo mitano kati ya kumi inayofaa kufuatwa katika kufuata kanuni za ulaji sahihi wa kila siku.

Wiki hii tunaendelea na miongozo ya mwisho mitano kama ifuatavyo:

6. kula milo mitano ya matunda kwa siku (5-A-DAY)
Hakikisha unafikia lengo la kula milo mitano ya matunda kwa siku, kiasi hicho ndicho kinachopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), lakini kiasi hicho ni cha kuanzia tu, unaweza kula zaidi ya hapo. Mlo mmoja ni sawa na kisahani kimoja cha chai, hivyo mwili unahitaji angalau visahani vitano vya matunda kila siku.

Aidha, unashauriwa kula mboga za majani katika kila mlo na kula matunda yenye rangi tofauti tofauti ili kupata virutubisho mbalimbali na muhimu kwa ustawi wa afya yako.

7. Epuka kukaanga vyakula (Skip Fry-up)
Epuka kula vyakula vya kukaanga, na kama ukilazimika kukaanga, basi usitumie mafuta yaliyobandikwa lebo ya 'vegetable oil', mafuta aina hii huharibika kirahisi yanapopata joto na hivyo kuwa si salama kiafya na huongeza kasi ya mtu kuzeeka!
Badala yake pendelea kuoka, kuchoma au kuchemsha vyakula. Ukilazimika kukaanga, basi tumia mafuta yaliyandikwa 'Olive Oil', 'Corn Oil' au 'sunflower oil' ambayo hayana madhara kiafya.

8. Kula mafuta mazuri (Eat 'good' fats)
Katika milo yako, tumia mafuta yaliyo bora, usiache kabisa kutumia mafuta, kwani mafuta nayo yana umuhimu wake katika mwili wa binadamu, ili mradi ni yale yaliyo katika kundi zuri.

Mafuta hayo mazuri utayapata kwa kula karanga, korosho, maparachichi, samaki, mafuta ya alizeti na nafaka, yote haya yameonesha kuwa na faida nyingi za kiafya, ikiwa ni pamoja na kuongeza kinga ya mwili, kulinda ubongo pamoja na moyo.

9. Punguza sukari (Kill the sugar).
Punguza kiwango cha sukari katika milo yako kwa kuepuka kula vyakula vilivyohifadhiwa kwenye makopo au paketi. Usipende sana kula keki, biskuti na vyakula vingine vya aina hiyo ambavyo huwa na kiasi kikubwa cha sukari. Badala yake pendelea zaidi kula matunda ya aina mbalimbali ambayo huwa na sukari nzuri itakayokusaidia kiafya mwilini.

10. Kula maharage (switch to beans)
Katika mlo wako, usikwepe kula maharage, njegele, njugu mawe na jamii nyingine za maharage kwani yana faida na umuhimu mkubwa katika mwili wa binadamu.

Maharage siyo tu yana kiasi kikubwa cha ufumwele (fibre), bali pia hayana kiasi kikubwa cha protein ambayo unaweza kuipata hata usipokula nyama, ambazo mara nyingi huwa zina kiasi kikubwa cha 'mafuta mabaya'.

Kwa ujumla ukizingatia mwongozo huu wa chakula, bila shaka unaweza kuishi maisha ambayo hutasumbuliwa na maradhi ya mara kwa mara.

Monday, August 13, 2007

BWANA HARUSI AJIUA SIKU YA NDOA!

Na Dotto Mwaibale aliyekuwa Chanika
Bwana harusi mtarajiwa, Jumanne Salehe Madeng'a (35) mkazi wa Kwangwale, Chanika jijini Dar es Salaam, amefariki dunia kwa kujinyonga kwa kamba ya katani aliyoifunga juu ya paa la nyumba yake huku akiwa amebakiza masaa machache afunge ndoa.

Kifo cha bwana harusi huyo kilichotokea juzi Jumapili, kimewasikitisha watu wengi waliokuwa wakimfahamu wakiwemo wazazi na mchumba wake aitwaye Jamila Saidi Msitu (30), kwani maandalizi yote ya sherehe hiyo yalikuwa yamekamilika ikiwa ni pamoja na kumtafuta sheikhe wa kufungisha ndoa hiyo.

Akiongea na mwandishi wetu aliyekuwepo eneo la tukio, mjomba wa marehemu, Bw.Mohammed Saidi alikuwa na haya ya kueleza:

''Kifo cha kijana wetu kimetusikitisha sana kwani alikuwa afunge ndoa leo hii (Jumapili) na maandalizi yote yalikuwa yamekamilika kwani chakula kilikuwa kimenunuliwa na kupikwa huku baadhi ya ndugu wanaoishi nje ya Dar es Salaam walikuwa tayari wamewasili.

"Mbali ya ndugu hao waliofika, jamaa wengine na marafiki wamepata taarifa za kifo hicho asubuhi hii wakiwa njiani kuja kwenye harusi huku akina mama wakiwa wamevaa sare za harusi.

"Siku ya Jumamosi asubuhi bwana harusi huyo mtarajiwa aliitwa na mama yake na kuambiwa kuwa leo asubuhi aende akachukue pesa kwa ajili ya kununua mboga ya sherehe hiyo.

"Baada ya kuambiwa hivyo aliondoka na hatukumuona tena hadi tulipopata taarifa hizo za kujinyonga leo hii asubuhi,"alisema Bw. Mohamed.

Naye mchumba wa marehemu, Jamila Saidi Msitu alisema kwamba Jumamosi mchana walikuwa na marehemu sehemu ya Msumbiji anakofanya biashara zake ambapo alimuaga kuwa anakwenda Gongo la mboto kumsalimia dada yake.

Alisema saa 12 jioni mchumba wake alimpigia simu akimjulisha kuwa amerudi na yupo nyumbani kwa mchumba wake huyo eneo la Masantula hapo Chanika.

Jamila alisema kwamba baada kufunga biashara yake alirudi nyumbani kwake ambapo alimkuta mchumba wake akiwa amejipumzisha, kisha walianza kuongelea juu ya ndoa yao iliyopangwa kufanyika leo saa nane mchana.

Alisema siku zote walikuwa na kawaida ya kwenda kulala nyumbani kwa mchumba wake, lakini siku hiyo aliambiwa kuwa hataweza kwenda naye kwa sababu kulikuwa na kaka yake aliyefika kutoka Kazimzumbwi kwa ajili ya harusi hiyo.

Baada ya kumuambia hivyo aliondoka ambapo alizima simu yake akaenda kulala na asubuhi alipoifungua alikuta ametumiwa ujumbe (sms) na mchumba wake akimuambia alale salama.
Alisema baada ya kusoma meseji hiyo aliamua kumpigia simu ili kujua maandalizi ya ndoa yao ambayo ilikuwa ifanyike siku hiyo, lakini ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa jambo lililomfanya apate wasiwasi ndipo alipomuita shemeji yake ambaye naye alipojaribu kupiga ilikuwa ikiita tu.

Wakati wakiendelea kumpigia, mama yake marehemu naye alikuwa akimpigia baada ya kuona amechelewa kwenda kuchukua pesa kwa ajili ya kununulia mboga, ndipo dada zake waliamua kwenda nyumbani kwa kaka yao ambako walikuta milango ikiwa imefungwa na walipopiga simu yake walisikia ikiita kutoka ndani.

Kutokana na hali hiyo waliingiwa na wasiwasi ambapo walikwenda kutoa taarifa kwa mjumbe wa nyumba 10 wa eneo hilo, Bw. Tullo ambaye alifungua mlango na kumkuta akiwa amejinyonga.

Habari zinasema mjumbe huyo alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Chanika ambao nao waliwataarifu wenzao wa Buguruni ambapo walifika eneo la tukio wakiwa na gari la polisi na. PT 0965 na kumkuta marehemu akiwa ananing'inia na walipopiga simu yake ilisikika ikiita kutokea sehemu zake za siri.

Askari hao walichukua maelezo kutoka kwa ndugu pamoja na ujumbe wa barua aliyoiandika marehemu na kisha waliondoka na mwili wake kwenda kuuhifadhi Hospitali ya Amana.

Ujumbe uliochwa na marehemu huyo ulisema ameamua kujiua kwa hiyari akiwa na akili timamu kwa sababu ya kutoelewana na ndugu zake katika mipango ambayo aliona haiendi sawa.

Katika ujumbe huo aliagiza nyumba, kitanda, godoro na mazao ya kudumu yaliyopo shambani mwake apewe mchumba wake.

Habari zilizopatikana kutoka kwa mmoja wa wana familia ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini, zimedai kuwa sababu ya bwana harusi huyo kuchukua uamuzi huo wa kujiua ni baada ya ndugu zake kung'ang'ania aoe siku hiyo baada ya kutoa mahari ambayo kwa kabila la Wazaramo wanaiita 'pamvu'.

Imedaiwa na ndugu huyo kwamba marehemu alitaka afunge ndoa mwezi ujao ili apate nafasi ya kualika marafiki zake walioko mbali na kufanya sherehe kubwa, lakini baada ya kuona jamaa zake wanamlazimisha ndipo aliamua kujiua.



'MTOTO HUYU ASIPOSAIDIWA HARAKA ATAKUFA'


Mariam Mndeme
Bi. Neema Paulo, mkazi Keko Magurumbasi jijini Dar es Salaam anaomba msaada kwa wasamaria wema kutokana na mwanae Mathew Pascal (pichani kulia) kukabiliwa na ugonjwa uliomfanya utumbo wake uwe nje.

Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Bi. Neema alisema mwanae huyo alizaliwa akiwa hana tatizo lolote lakini baada ya wiki moja alianza kuvimba tumbo ambapo sasa anaona asiposaidiwa anaweza kufa.

Alisema kuwa baada ya mwanae huyo kuvimba tumbo alimpeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo alifanyiwa upasuaji na kuachwa utumbo aina mbili nje ukining'inia hivyo kumpa wakati mgumu wa kumlea mtoto huyo.

Aliongeza kuwa baadae alitafuta fedha na kumpeleka mtoto huyo kwa mara nyingine Hospitali ya Muhimbili ambapo alifanyiwa upasuaji wa kuingiza ndani utumbo mmoja na kubaki mmoja na sasa amekwama kutokana na ukata.

"Nawaomba Watanzania wenzangu wanisaidie ili mtoto akafanyiwe upasuaji wa kuuingiza utumbo uliobaki ndani, naamini zoezi hilo likifanyika ataishi kama watoto wengine, nawaomba mnisaidie mwanangu anakufa, sielewi kwanini awali madaktari waliuacha utumbo huu mmoja nje," alisema kwa masikitiko mama huyo.

Yeyote aliyeguswa na habari hizi awasiliane kwa simu namba +255 0754 325 939 au wanaoishi Dar es salaam wafike ofisi za gazeti hili Mtaa wa Aggrey, jengo la vioo, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

CHAHALI AJIBU!

DEAR ABDALLAH MRISHO (General Manager,Global Publishers),

DEAR SALUM MNETTE(Editor,RISASI Newspaper)

DEAR TULIZO KILAGA (Sub-Editor,Global Publishers),



LET ME SET THE RECORD STRAIGHT.THE FOLLOWING PARAGRAPH,WHICH APPEARED ON AUG 8,2007 IN MY COLUMN IN A DAILY PAPER“KULIKONI,” AND A POST IN MY BLOG (http://chahali.blogspot.com/2007/08/kulikoni-ughaibuni-74.html) COULD HELP IN SHADING A LIGHT ON WHO SPEAKS THE TRUTH IN THE ON-GOING BROUHAHA.IT READS AS FOLLOWS :

Jingine lililonikera ni gazeti la RISASI ambalo katika toleo lake la Julai18-20 lilikuwa na habari kwamba “Warembo TZ wapiga picha za X tupu…zasambazwa mitaani,baadhi yao ni washiriki wa kusaka mataji ya u-miss.” Kinachosikitisha sio kama iwapo habari hiyo ni ya kweli au ya kubuni bali ni picha zilizotumika kwenye habari hiyo.Rafiki yangu mmoja aliyeko Marekani amenifahamisha kuwa wasichana walioko kwenye picha hizo ni wacheza filamu za ngono (porn stars) wa Marekani na wala sio Watanzania.Kwa kuthibitisha alichokuwa anasema,alinipatia tovuti ambazo zina picha za Wamarekani hao weusi.Kama picha zilizotumiwa na RISASI ni feki basi yayumkinika kusema kuwa hata habari yenyewe ni feki.Hivi ni uzembe wa mhariri kucheki ukweli wa habari husika au ndio kuwafanya Watanzania wajinga kwa kuwapa habari “sensational” ambazo hazina ukweli?Nyie ni watu wazima ambao mmeshatengeneza faida ya kutosha kwa kuandika udaku lukuki wa kweli,sasa tamaa ya nini hadi mfikie hatua ya kunyofoa mapicha kwenye mtandao na kuzusha habari?Shame on you!

IF YOU READ CAREFULLY BETWEEN LINES YOU WILL UNDOUBTEDLY UNDERSTAND THAT I WASN’T ACTUALLY CONTESTING CREDIBILITY OF YOUR STORY BUT RATHER AUTHENTICITY OF THE PICTURES ACCOMPANYING THE STORY (refer to the first underlining).I ALSO MADE IT CLEAR THAT BEFORE CRITICISING YOU IN “KULIKONI”,I DID CHECK THE PHOTOS’ LINKS I WAS SENT BY MY FRIEND,AND IT’S ONLY WHEN I WAS 105% SATISFIED THAT YOU INTENDED TO DECEIVE YOUR READERS BY USING FAKE PICTURES FROM THE INTERNET,THAT I DECIDED TO INCLUDE THAT MATTER IN MY COLUMN. YOU DON’T EVEN HAVE TO HOLD A SHORT COURSE CERTIFICATE IN JOURNALISM TO UNDERSTAND THAT BY USING DOCTORED,ENGINEERED OR FAKE PICTURES IN A STORY YOU SURELY JEOPARDIZE IT’S,AND THEREFORE YOUR PAPER’S,CREDIBILITY.SOME OF THE LINKS,WHICH I DIDN’T INCLUDE IN MY ARTICLE DUE TO THEIR EXPLICIT NATURE,ARE AS FOLLOWS:

http://www.wannawatch.com/hosted/index.php?wsc/xnxxporn/tinysblackadventures63
http://www.wannawatch.com/hosted/index.php?wsc/xnxxporn/tinysblackadventures75
http://www.bikinidream.net/gals/glam0049/15.jpg
http://www.bikinidream.net/gals/glam0049/index.php?id=110154

NOW LET’S GO BACK TO YOUR STORY IN RISASI (http://abdallahmrisho.blogspot.com/2007/07/wabongo-na-picha-za-x.html ).YOU CLAIMED “Warembo wa Tanzania waliojitambulisha kwa jina moja moja la Amina, Janie na Candy wamepiga picha za utupu (x) na kuzisambaza sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam IMPLYING THAT IT’S THE SAID TRIO WHO INTRODUCED THEMSELVES TO YOU,AND FOR THAT MATTER IT GOES WITHOUT SAYING THAT YOU NEVER HAD A CHANCE TO PROVE WHETHER THEY WERE REALLY THE ONES IN THE PICTURES YOU HAD OR THEY WERE JUST USING THEM FOR COMMERCIAL PURPOSES.YOU WENT ON CLAIMING THAT “Kwa upande mwingine gazeti hili liliamua kufungua mitandao iliyoainishwa katika picha hizo na kukuta mambo ya kusikitisha. BUT IF YOU WERE CAREFULLY ENOUGH YOU’D HAVE EASILY NOTICED THAT AT http://swallowmyjuice.hi5.com/ THERE WAS NO AMINA,JANIE OR CANDY.THE PAGE BELONGS TO SOMEONE CALLING HERSELF “MELANIE,” BUT THAT’S,IN FACT,LORI ALEXIA’S PICTURE.JUST GOOGLE THE NAME AND YOU’LL SURELY DISCOVER THAT SHE’S NOT A TANZANIAN BUT AN AMERICAN OF BARBADOS ORIGIN.FURTHERMORE YOU WROTE THATKatika mitandao hiyo warembo hao wameweka bei za huduma wanazozitoa na pindi mteja anapokubaliana nazo humtumia picha mbalimbali za utupu ili kumshawishi BUT IN MELANIE’S (LORI) PAGE THERE’S NO SUCH INFORMATION (“bei za huduma”).MOREOVER,THE GIRLS ARE USING THE NAMES MELANIE,GRACE AND SUSSANE (WHO CLAIMS TO BE,NOT A TANZANIAN,BUT A UGANDAN BISEXUAL FROM KAMPALA),AND NOT AMINA,JANIE OR CANDY AS YOU SENSATIONALLY ASSERTED.

IN YOUR “TAARIFA MAALUM KWA CHAHALI,GAZETI LA KULIKONI” (http://abdallahmrisho.blogspot.com/2007/08/taarifa-maalum-kwa-chahali-gazeti-la.html) YOU CHARGED THAT “Tunapenda kumfahamisha Chahali kuwa sisi hatuna haja ya kutunga habari ‘sensational’ wakati hizo zipo nyingi katika jamii tunayoishi na kama yeye hazijui haina maana kuwa hazipo. Hivi inawezekana kweli yeye tu ndiye awe ameiona habari ile ni ya uongo miongoni mwa mamilioni ya Watanzania wa ndani na nje ya nchi walioisoma?” IT’S THE UNDERLINED SENTENCE THAT MADE ME WONDER WHETHER YOU WERE REALLY SERIOUS OR SIMPLY KIDDING WHEN WRITING THE “TAARIFA MAALUM.” HOW ON EARTH DID YOUR KNOW THAT MILLIONS OF TANZANIANS WHO READ THE STORY DID ACTUALLY BUY (BELIEVE) IT?IT TOOK ME ABOUT THREE SOLID WEEKS TO COMMENT IN MY COLUMN ABOUT THE PHOTOS WHICH ACCOMPANIED YOUR STORY.WHY ALL THAT LONG?SIMPLY BECAUSE I ONLY CRITICIZE WHEN I HAVE ENOUGH EVIDENCE THAT MY SUBJECT TRULY DESERVE SUCH CRITICISM.AS TO WHY DIDN’T OTHER “MILLIONS OF TANZANIA” REACT THE WAY I DID,SIMPLE REASON MIGHT BE THEY JUST IGNORED IT,OR SOME WERE,TOO, TRYING TO ESTABLISH THE FACTS BEFORE CRITICIZING YOU (ONE HAS TO,BECAUSE YOU DON’T SEEM TO TAKE ANY SORT OF CRITICISM “LIGHTLY.”).SILENCE DOESN’T ALWAYS NECESSARILY MEAN INACTION.

ALTHOUGH YOU SEEM TO HAVE BEEN STAUNCHEST BELIEVERS OF AN OLD ADAGE THAT “OFFENCE IS THE BEST FORM OF DEFENCE” BY QUESTIONING AND DISCREDITING MY ACADEMIC CREDENTIALS AND PROGRESS,(WHICH HAS AS A RESULT SEVERELY AFFECTED NOT ONLY MYSELF BUT ALSO MY SPONSOR-CUM-EMPLOYER,FAMILY,FRIENDS AND RELATIVES),MY SOLE INTENTION AT THIS JUNCTURE IS TO PUT THE RECORD STRAIGHT.I AM IN NO WAY WHATSOEVER SEEKING FOR CHEAP POPULARITY OR INSTANT FAME AT YOUR EXPENSE,AS IT HAS BEEN SUGGESTED.MY ARTICLES IN “KULIKONI”,AND THEIR ARCHIVAL FORM IN A BLOG (chahali.blogspot.com), ENJOY A WIDER READERSHIP WITHIN AND BEYOND TANZANIA.I COMPLETELY REFUTE THE ALLEGATION THAT I VIEW TABLOIDS SUCH AS “IJUMAA” AND “RISASI”,AS USELESS,RUMOUR MONGERS OR GOSSIP-PRONE.HAD THAT BEEN THE CASE,I WOULD HAVE NEVER EVEN COME ACROSS THE CONTESTED STORY IN “RISASI.” BY THE WAY,EVEN HERE IN THE UK,ONE OF BEST-SELLING PAPERS IS A TABLOID TOO (THE SUN).TABLOID OR NOT,ANY PAPER’S REPUTATION RESTS IN THE HANDS OF PEOPLE BEHIND IT (OWNER,EDITOR,REPORTERS,ETC ETC).THE MORE SERIOUS THESE “BRAINS” ARE,THE HIGHER THE REPUTATION,AND THE MORE “UJANJAUJANJA” AND “USANII” A PAPER ENTERTAINS,THE MORE CRAPPY IT LOOKS IN THE PUBLIC EYES.

FINALLY,I WOULD REALLY APPRECIATE IF YOU COULD PUBLISH THIS E-MAIL IN YOUR BLOG,JUST AS I DID TO YOURS IN MINE.THAT COULD HELP THE PUBLIC IN SIEVING FACTS FROM MANUFACTURED FICTION.

SINCERELY YOURS,

EVARIST CHAHALI
49 TILLYDRONE AVENUE
ABERDEEN
AB24 2TE
TEL +44 1224 491 773
MOB +44 7814 483 356
UNITED KINGDOM

..........................................

Majibu ya editors wa Risasi kuhusu hoja hii na kwa wachangiaji wote, tangu mjadala huu ulipoibuka, yatachapishwa leo baadae na kuweka mambo yote sawa na kila mmoja atajua Chahali alikosea wapi na alitukera wapi....stay tuned!

N.B kwa Chahali: kwa mara ya kwanza nimeiona email yako leo asubuhi hii kutoka source nyingine, japo umedai kuwa tumekuwa tukikubania, hujawahi kuipost kwenye blog hii wala kunitumia kwenye email yangu wala za editors wa Risasi, kwani hatujawahi kuiona na wala sina sababu ya kuacha kuipost hapa- Mrisho

Sunday, August 12, 2007

NGONO KWENDA MBELE!!


RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA
kamera ya Ijumaa Wikienda ikiwa kazini, wikiendi iliyopita iliwanasa njemba moja na mrembo aliyefahamika kwa jina la Prisca Michael wakifanya vitendo vya ngono uchochoroni.

Fumanizi hilo lilitokea usiku wa manane wa kuamkia Jumamosi, katika moja ya vichochoro vilivyopo karibu na Klabu ya High Way Night Park ‘Kwa Macheni’, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Timu ya Wikienda ambayo ilikuwepo maeneo hayo, ikikusanya matukio yanayojiri usiku huo ili kuijuza jamii, ilifuatilia kwa karibu ‘mkandamizo’ huo bila kupoteza pointi hata moja.

Kabla ya fumanizi, aliyekuwa wa kwanza kuonwa na waandishi wetu ni Prisca ambaye alikuwa akizunguka zunguka katika maeneo jirani na klabu hiyo kana kwamba alikuwa akitafuta kitu.

Majira ya saa saba na dakika kadhaa za usiku, ilitokea njemba hiyo ambayo haikufahamika jina mara moja na kuanza kuongea na Prisca, maongezi ambayo timu yetu haikufanikiwa kuyanasa.

Hata hivyo, maongezi kati ya wawili hao hayakuchukua muda mrefu, kwani kitambo kidogo, walishuhudiwa wakiongozana kuelekea gizani. Timu yetu, baada ya kuvutiwa na mkanda huo, ilijigawa na kuanza kufuatilia nyendo za Prisca na mwenzake ili kujua mwisho wao.

Aidha, waandishi wetu wakiwa wameandaa kamera tayari kwa kazi mbele yao, waliweza kuwaona wawili hao wakiwa wamejibanza uchochoroni huku wamekumbatiana. Bila kufanya ajizi, kamera yetu ikiwa mbali kidogo kutoka walipokuwa Prisca na mwenzake, ilifanikiwa kupata picha nne zilizopigwa bila kushtukiwa.

Baada ya kukamilisha zoezi la upigaji picha, timu ya gazeti hili iliwasogelea wawili hao kwa lengo la kuwauliza sababu ya kufanya vitendo hivyo uchochoroni, lakini njemba hiyo ilitimua mbio baada ya kujua kwamba watu waliokuwa mbele yake ni waandishi wa habari.

Hata hivyo, ilifanikiwa kumpata Prisca ambaye kabla ya yote alianza kulaumu kwa kukimbiziwa mteja wake. “Nyie wadaku vipi? Mbona mnaingilia anga za watu? Mnaona mpaka mteja wangu amekimbia, bahati yenu ameshanipa changu, vinginevyo tungekabana mashati,” alifoka Prisca.
Mrembo huyo ambaye alikuwa amekolea kilevi aliongeza: “Msione watu wanapeana raha, nyie mnawashwa, haya semeni kama mnataka ‘mchezo’ niwasaidie.”

Alipoulizwa kwa nini alikuwa akifanya mapenzi uchochoroni, mrembo huyo alijibu kwamba hakuna mtu anayeweza kumpangia. “Mapenzi popote, kama aibu mnazo nyie, mimi naangalia biashara, nakubaliana na mtu wangu, tunazama sehemu yoyote anayotaka, kama hana hela ya gesti je, nyie vipi?” Alihoji mrembo huyo.

Hata hivyo, baada ya kutuliza munkari, mrembo huyo alisema, hafanyi biashara ya kuuza mwili kwa shida kwa sababu anatoka kwenye familia inayojiweza kifedha. Alisema, anafanya ukahaba kama ‘hobi’ na kuongeza kuwa wazazi wake wameshajitahidi kumfanya aache lakini imeshindikana.

“Nyumbani kwetu ni Kimara, mimi naitwa Prisca Michael, baba yangu ni mtu mwenye uwezo tu, kwahiyo msinione hapa mkadhani labda shida ndiyo zimenifanya niwe changudoa,” aliongeza mrembo. Baadaye, waandishi wetu walimpiga picha mrembo huyo akiwa amepozi, baada kuomba afanyiwe hivyo kwakuwa endapo ataonekana gazetini, basi wateja wataongezeka.

Huu ni uchafu ambao haupaswi kufumbiwa macho, Ukimwi unazidi kushika kasi, lakini miongoni mwa tabia hatarishi za ugonjwa huo ni biashara ya ngono. Jamii bado inahitaji kuelimishwa zaidi ili yapatikane mapinduzi ya fikra, vitendo vinavyofanyika usiku vinatisha, hatuwezi kuzuia Ukimwi kama tunafumbia macho uchafu utokeao usiku. Mhariri



Mariam Mashauri aeleza yaliyomkuta gerezani

Wanza Temu na Imelda Mtema

Aliyekuwa Mshiriki wa Shindano la Muziki la Bongo Star Search (BSS) mwaka 2006-07, Mariam Mashauri, ameeleza yaliyomkuta gerezani sambamba na kusimulia picha halisi ya maisha ya mfungwa wa kike.

Kwa mujibu wa mahojiano kati ya waandishi wetu na mwanamuziki huyo, Ijumaa iliyopita jijini Dar es Salaam, Mariam pia alimshukuru Mungu kwa kuachiwa huru ikiwa ni miezi mitatu tangu alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.

Mariam ambaye alikuwa katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, aliongea mambo kadhaa kuhusiana na maisha ya ufungwa, katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni B, ikiwa ni saa kadhaa baada ya kuachiwa huru.

Mahojiano hayo yalikuwa kama ifuatavyo;
Wikienda: Habari yako Dada Mariamu na hongera kwa kuachiwa huru.
Mariamu: Ahsante sana, namshukuru Mungu yeye ndiye muweza wa yote.

Wikenda: Sisi ni waandishi wa habari kutoka Gazeti la Ijumaa Wikienda, kwanza tunakupa pole kwa matatizo yaliyokupata, lakini ni vizuri kama utatueleza unajisikiaje kuwa huru na imekuwaje leo umeachiwa?

Mariamu: Ahsanteni, nimeachiwa kwa sababu baada ya kuhukumiwa, nilikata rufaa kwa sababu sikutendewa haki kwenye hukumu ya kwanza, kwahiyo nimeshinda, mimi ni Mtanzania na cheti cha kuachiwa hiki hapa (anawaonesha waandishi).

Wikienda: Unadhani nini chanzo cha kuenea habari kwamba wewe siyo Mtanzania na kusababisha ukafungwa?

Mariamu: Watu siyo wazuri, wapo wasiopenda maendeleo yangu, wanasema lafudhi yangu, lakini hiyo ni kuongea tu wala haina maana kuwa mimi ni mgeni wa nchi hii, chanzo cha hayo yote ni rafiki yangu mmoja, yeye ndiye aliyenichongea hadi nikapata matatizo yote, ukweli ni kwamba mimi ni Mtanzania, baba yangu ni Msambaa wa Tanga ila mama ni Mzambia.

Wikienda: Kwa maana hiyo unamjua adui yako, sasa unatarajia kuchukua hatua gani dhidi yake?

Mariamu: Nimeshamsamehe, sitochukua hatua yoyote, haki ipo mbele ya Mungu peke yake.

Wikienda: Zipo taarifa ambazo zimezagaa kila kona kuhusu jela kwamba kuna vitendo viovu, ushoga kwa wanaume, usagaji kwa wanawake, uvutaji wa bangi na wafungwa wa kike kulazimishwa ngono na askari magereza wa kiume, je, wewe yalikukuta hayo?

Mariamu: Namshukuru Mungu sana, mimi sikuwahi kukutana na vitendo hivyo, huwa nasikia hata nilipokuwepo gerezani nilisikia watu wakisema mambo hayo, lakini haikutokea kwangu, Mungu ni mkubwa, alinikinga kwa yote.

Naweza kusema jela imenisaidia kwa kiasi fulani, imenifunza mambo mengi, kule kulikuwa na ngoma ya gereza, kwahiyo nilikuwa nacheza sana, pia nimejifunza kushona masweta na mambo mengine.

Wikienda: Kuna vitu gani ambavyo vilikuwa vikikukwaza katika kipindi chote cha miezi mitatu uliyokuwepo gerezani?

Mariamu: Washiriki wenzangu katika Shindano la Bongo Star Search hawakuja kuniona hata siku moja, kwa kweli ilinisikitisha sana kuona hata majaji wetu hawakunijali angalau kuja kunipiga jicho hata mara moja, hata hivyo, sina kinyongo, nimewasamehe wote.

Wikienda: Ukiambiwa utaje vitu ambavyo utavikumbuka sana gerezani, utaorodhesha nini na nini?

Mariamu: Mimi nilikuwa nikitunga nyimbo na kuimba, mpaka sasa nina albamu yangu ambayo imekamilika kwa nyimbo tano, pia wafungwa wenzangu, niliwazoea sana, mimi nilikuwa mpole kwahiyo nilielewana na kila mtu, wakawa wakarimu kwangu, niliwafundisha kumjua Mungu na kutubu dhambi na leo nilipowaaga, wengi wamelia machozi.

Wikienda: Vipi 'msosi' wa gerezani, ulikuwa unapanda au ulikuwa ni adhabu kwako?

Mariamu: Nilikuwa nakula chakula bila kudengua, nilijua kila kitu ni mapito tu.

Wikienda: Tunafurahi upo huru tena, tunakupongeza, lakini tunataraji kukuona ukiwasha moto mkali kwenye fani yako ya muziki.

Mariamu: Ahsante, kazi ipo.

WADAU WA UREMBO BONGO: MNAMKUMBUKA MREMBO HUYU?


Leo Abby Cool & MC Geroge Over The Weekend imeamua kukufanyia bonge la surprise, imetega na mitego imemnasa na kumuibua Miss Tanzania namba 2 mwaka 1999 - 2000, Ayan Hassan(pichani juu) kisha kupiga naye stori.

Akiongea kupitia mtandao wa internet, mnyange Ayan alisema kwamba, muda mrefu aliotoweka nchini yupo kwenye ardhi ya Malkia Elizabeth, UK, akilisongesha gurudumu la maisha na amekuwepo nchini humo kwa miaka mitano sasa.

Aidha mlimbwende huyo aliyepata kutingisha kunako sanaa ya urembo alisema kuwa, akiwa nchini humo tayari ameshamaliza masomo yake ngazi ya diploma, yaliyomgharimu miaka mitatu katika chuo cha Hammersmith and West London cha London, England na sasa hivi anajipanga kwenda kutembea USA.

Pia nina mpango wa kurudi nyumbani na ninamatumaini ya kufungua biashara yangu mwenyewe, japo sijaamua nifanye bishara ya aina gani. Kuhusu masuala ya urembo kwasasa nimeyaweka kando, sina mpango wa kuendelea na mambo ya urembo kwa sasa, labda baadaye.

"Ningependa kuwashauri washiriki wa urembo wajitahidi kujihadhari na gonjwa la ukimwi. Ningewaomba kwakuwa wao ni jicho la umma wawe mstari wa mbele katika kuielimisha jamii kuhusu HIV hasa vijana."Rais Kikwete (Jakaya) kashatoa mfano naomba tumuunge mkono", alisema Ayan Hassan.

USIKU WA TWANGA, JAMAA ZIII!

Iron Lady.. mamaa Asha Baraka akifuatilia vijana wake wa African Stars huku akiteta na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mh. Juma Kapuya..!
Jamaa ziii'''ndani ya Mango Garden, usiku wa Twanga Pepeta...ina kuwaje!

AROBAINI YA AMINA, VILIO VYAIBUKA UPYA!

Marehemu Amina Chifupa, kipenzi cha wengi, jana alitimiza siku arobaini tangu aiage dunia na katika kisomo cha arobaini hiyo kilichofanyika nyumbani kwa mzee Chifupa Mikocheni vilio viliibuka tena wakati ndugu na jamaa walipokutana tena. Mungu ailaze roho ya marehemu peponi, DAIMA ATAKUMBUKWA!
Mama mzazi wa Amina akiwa katika majonzi mengine ya kumkubuka kipenzi chake wakati wa Arobaini ya mwanae jana jijini Dar es salaam.
Familia ya Mpakanjia, kati ni mama mzazi wa Meddy, mtoto anayeiangalia kamera ndiye Rahman mtoto wa marehemu Amina. Meddy mwenyewe hakuhudhuria arobaini hiyo na kuna habari zinasema 'yu mgonnjwa'.
Mzee Chifupa (kushoto) akiwa na kaka yake pamoja na 'daruwesh' maarufu jijini Dar (kulia) kwenye Arobaini ya marehemu Amina

Saturday, August 11, 2007

VITUKO VYA 'GOAT RACE'

Mbuzi wa kijana Hassan Mpole ndiye aliyeibuka mshindi katika mashindano ya mbio za Mbuzi yaliyofanyika Leaders Club jijini Dar es slaam Jumamos mchana. Mbuzi nambari nne mgongoni aliibuka na kitita cha 1.2m za bongo!
Mshike mshike wa mbio za mbuzi, Leaders Club Jumamosi mchana
Hawa ni 'minjemba', usidhani ni akina aunt, kundi lao linajiita AYAM GOAT RACING na ndio wenye mashindano haya bongo

Taarifa maalum kwa Chahali, gazeti la Kulikoni

Kampuni ya Global Publishers & General Entreprises wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Amani, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Championi na Risasi, imesikitishwa sana na makala iliyoandikwa katika Gazeti la Kulikoni linalotolewa na Kampuni ya Media Solutions Ltd ya jijini Dar es Salaam.

Makala hayo yaliyochapishwa katika toleo lake la Jumatano ya Agosti 8, mwaka huu, yaliyokuwa na kichwa cha habari ‘Magazeti ya Udaku yanaandika habari feki’, iliushutumu uongozi wa gazeti hili kuwa waliandika habari ya uongo katika toleo lake la Julai-20, mwaka huu.

Habari ambayo mwandishi huyo alidai kuwa ni ya uongo ilikuwa na kichwa kisemacho, ‘Warembo wa TZ wapiga picha za X tupu’.

Pamoja na shutuma hizo, Kulikoni pia kupitia kwa mwandishi wake anayejiita Evarist Chahali, mwanafunzi Mtanzania anayesoma katika Chuo cha Aberdeen, nchini Scotland, lilidai kuwa, mhariri alitumia picha za wasichana watatu ambao alielezwa na rafiki yake kuwa ni wacheza filamu za ngono (Porn stars) nchini Marekani na si Watanzania wanaojiuza kama gazeti hili lilivyoandika.

Kupitia makala yake, mwandishi huyo amediriki pia kulishambulia gazeti hili waziwazi akidai kuwa yeye binafsi linamkera sana kwani linaandika habari za kuzusha.

Maelezo aliyoandika mwandishi huyo kwa kweli yanatufanya tuamini kuwa, digrii alizonazo zina mashaka kutokana na kushindwa kwake kufanyia uchunguzi wa kutosha kabla ya kufikia hatua ya kutoa shutuma kama hizo zenye lengo la kuchafuliana.

Kwa ujumla, tungependa kusisitiza kuwa habari iliyoandikwa kwenye gazeti hili ni ya kweli na kwamba wasichana waliochapishwa wametambulishwa katika mtandao huo kuwa ni watanzania wanaojiuza kwa njia ya kupiga picha chafu na si Wamarekani kama alivyodai Chahali.

Tunaamini kuwa Chahali ni msomi, hata kama si katika nyanja ya uandishi, hivyo hakupaswa kuandika shutuma zile baada ya kumnukuu mtu kwa maneno ambayo hakuyafanyia uchunguzi, kwani hatua hiyo inaweza kumfanya ashindwe kuthibitisha mbele ya sheria.

Kimsingi picha za wasichana waliochapishwa kwenye gazeti hilo ni Watanzania kama walivyojieleza wenyewe kupitia tovuti ambayo tumelazimika kuiweka wazi mwisho wa taarifa hii, ili kuuthibitishia umma kuwa hatuandiki, hatujaandika na wala hatutaandika habari ‘feki’.

Chahali anapaswa kuelewa kwamba habari tuliyoiandika haikuwa jambo geni sana ambalo haliwezi kufanywa na Watanzania wa leo, hayo mambo yapo, tena mengine ni mazito zaidi na hayaandikiki kwenye gazeti.

Aidha, asifikiri wasomaji wetu ni wajinga ambao wanaweza kudanganywa kirahisi kwa kuwaandikia habari za uongo. Hayo ni mambo ya kawaida katika jamii yetu hivi sasa, lakini Chahali anaonekana kuwa ni mgeni wa maendeleo ya sayansi na teknolojia kwa kufikiri kwamba kitu kama hicho kinafanywa na Wamarekani pekee.

Tunapenda kumfahamisha Chahali kuwa sisi hatuna haja ya kutunga habari ‘sensational’ wakati hizo zipo nyingi katika jamii tunayoishi na kama yeye hazijui haina maana kuwa hazipo. Hivi inawezekana kweli yeye tu ndiye awe ameiona habari ile ni ya uongo miongoni mwa mamilioni ya Watanzania wa ndani na nje ya nchi walioisoma?

Tunawaheshimu sana wasomaji wetu na wao ndio vyanzo vyetu vikuu vya habari tunazoziandika. Chahali anapaswa kuelewa kwamba tunachokiandika, siku zote huwa kinatoka kwa wasomaji hao na ndio maana wamekuwa wakituamini kwa miaka karibu kumi sasa.

Kwa kumrahisishia kazi Chahali na kumjuza kuwa hatuna sababu ya ‘kutunga’ habari ili tupate pesa, atembelee tovuti hii: http://swallowmyjuice.hi5.com ili akajionee mwenyewe wasichana hao anaodai ni Wamarekani, ili siku nyingine aache kuropoka na kuingilia mambo ya watu asiyoyajua.

Hatukatai kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake ilimradi havunji sheria, lakini si vizuri kutoa shutuma nzito dhidi ya mtu mwingine kwa chuki binafsi na ‘roho ya kwa nini’, kama vile ambavyo Chahali mwenyewe amesema katika makala yake, eti ‘mmeshatengeneza faida ya kutosha’!

Kimsingi magazeti ya Udaku yanafanya kazi sambamba na vyombo vingine katika kupasha habari, kuelimisha na kuburudisha jamii na kwamba hayapo Tanzania tu bali hata katika nchi nyingine kama Uganda, Marekani, Uingereza na kwingineko na yanapendwa kama yanavyopendwa ya hapa nchini.

Mwisho, kwa taarifa hii tunawaomba wahariri wa Kulikoni, ambao tunawaheshimu sana, kuwa makini na waandishi wanaotaka kutumia gazeti hilo kwa manufaa yao binafsi kwa lengo la kuchafuliana na kushushiana hadhi mbele ya jamii.

Imetolewa na kusainiwa na:
Abdallah Mrisho
Meneja Mkuu
Global Publishers & General Enterprises Ltd

CHAHALI, VYA KUMUNG’UNYA UNATAFUNA, INAKUWAJE?

Na Tulizo Kilaga
(MAKALA MAALUM KWENYE GAZETI LA RISASI -AGOSTI 11,2007)

JUMATANO ya wiki hii, yaani Agosti 8, 2007 nilisoma, nikashtuka, nikapata uchungu kutokana na makala iliyoandikwa na Evarist Chahali, iliyokuwa na kichwa cha habari ‘Magazeti ya Udaku yanaandika habari feki’. Nililazimika kusoma makala hayo zaidi ya mara tano na kila nilipofika kwenye neno “ shame on you!” niligadhabika na kutafuta nguvu ya kujenga hoja, hatimaye nikajiridhisha na sasa naomba niweka sawa haya yafuatayo.

Evarist Chahali amedhihirisha wazi kuwa ana uelewa mdogo katika uandishi, anadhani kujua kusoma na kuandika pekee kunatosha mtu kuwa mwandishi, najua wapo wengi wasioamini kuwa uandishi ni taaluma kama huyu mkurupukaji Chahali, hivyo nataka niwathibitishie kuwa uandishi ni taaluma.

Binafsi nimefadhaishwa sana na maneno nitakayoyanukuu hapa chini kutoka kwenye makala yake “Hivi ni uzembe wa mhariri kucheki ukweli wa habari husika au ndiyo kuwafanya watanzania wajinga kwa kuwapa habari “sensational” ambazo hazina ukweli? Nyie ni watu wazima ambao mmeshatengeneza faida ya kutosha kwa kuandika udaku lukuki wa kweli, sasa tamaa ya nini hadi mfikie hatua ya kunyofoa mapicha kwenye mtandao na kuzusha habari? Shame on you!”

Mwandishi huyo amesahau kuwa Risasi ni gazeti lenye jukumu kubwa la kuhakikisha linaipa jamii habari iliyo sahihi na ya kuaminika.

Nikiwa kama mhariri msaidizi wa gazeti hili, nasema Chahali ni muongo! Amenisikitisha kwani mtu mzima kuanza kuzusha na kusema uongo kwa faida ya vitu vidogo vidogo vyenye shibe ya kitambo, ni mambo ya kuhuzunisha na kujidhalilisha.

Mimi nasema kuwa, Chahali kwa elimu yake kubwa, alipaswa kujua kuwa katika kutoa hoja mtu anatakiwa kufuata taratibu za fikra sahihi na si vionjo kama alivyofanya!

Nakumbuka vema katika miaka mitatu niliyokesha kutafuta Shahada yangu ya kwanza katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini- Iringa Mkufunzi wangu wa Physchologia Marehemu Prof. Samuel Mshana (Mungu amlaze mahala pema peponi) alipenda kunisisitizia maneno ya mwanafalsafa Plato kuwa ulimwengu umegawanyika katika makundi mawili, yaani ulimwengu wa busara na akili na ulimwengu wa muonekano/maoni.

Kimsingi Plato anamaanisha kuwa wale wenye busara na fikra sahihi wapo kwenye ulimwengu wa ukweli na wale wenye vionjo kama Chahali wapo kwenye ulimwengu wa maoni!

Chahali ni mchangiaji wa habari katika gazeti la Kulikoni anayeishi Scotland, nchini Uingereza ambako anasomea Udaktari wa Falsafa katika Siasa za Kimataifa, hususan kuhusu Afrika na anafanya utafiti kuhusu Uislam na harakati za vikundi vya Kiislam nchini Tanzania.

Huyu ni msomi kwani alipata Shahada ya Kwanza katika Elimu ya Jamii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ‘Mlimani’ kabla ya Kupata Shahada ya Uzamili katika Siasa na Uhusiano wa Kimataifa kisha kufuatiwa na Shahada ya Uzamili wa Utafiti (Master of Research-MRes) katika Utafiti wa Siasa (Political Research) huko aliko sasa.

Hakika Chahali ni msomi lakini kuna maswali mengi najiuliza, hivi huyu ni msomi wa aina gani, anayethubutu kuandika makala bila kuifanyia uchunguzi? Mbaya zaidi ndugu yangu ana taaluma ya Shahada ya Uzamili wa Utafiti, lakini hataki kwa makusudi kuitumia! Msomi wa namna hii ni sawa na mwandishi asiyeweza kuona mwanga gizani.

Nakumbuka siku namaliza shahada yangu ya uandishi wa habari, mkufunzi wangu aliyekuwa akinifundisha ‘teaching methodology’ Fredy Nyamubi aliniambia kuwa, ili ujue elimu uliyonayo inakusaidia ama umeelimika lazima uweze kutumia taaluma ulionayo katika maisha yanayokuzunguka. Hivyo, kila ninapotaka kufanya kazi zangu huyakumbuka maneno haya.

Chahali anapaswa kujua kuwa, zipo kanuni zinazomuongoza mwandishi yeyote kuweza kupata habari iliyo sahihi, hivyo ukitumia vema kanuni hizo pamoja na mambo kadhaa ya msingi yanayoifanya habari kuwa habari, basi habari itakayoandikwa huwa sahihi.

Tasnia ya habari duniani kote huzingatia kanuni nne ambazo ni ukweli, utii, uthibitisho na kuwa na imani na unachokiandika, hivyo Chahali lazima azingatie kanuni hizi, lakini kwa kuwa watanzania hawana utamaduni wa kujisomea wanaweza kupata Gazeti la Rai la Alhamisi ya Juni 28 – Julai 4, 2007 Uk. 9 ambapo kuna makala iliyoandikwa na mkongwe wa habari, Muhingo Rweyemamu.

Katika makala hiyo Rweyemamu anasema “Uandishi wa habari una tofauti na uandishi wa barua au malalamiko. Anayelalamika hata kama analalamika kwa rais, hana sababu ya kumpa nafasi anayemlalamikia vivyo hivyo kwa mwandishi wa barua.”

Nirudi kwa Chahali, hivi ni kweli hajui kuwa nidhamu ya msingi ya mwandishi wa habari duniani kote ni ile inayompa nafasi mtuhumiwa? Sitaki kuamini kuwa nawe ni miongoni mwa watu wanaoamini nidhamu hii huitajika kwenye habari kubwa ya kuuzia gazeti tu! Hata makala hutakiwa kuzingatia hili kwani nayo ni habari.

Hainiingii akilini, kwanini Chahali hakutaka kutoa nafasi kwa wahariri wa gazeti hili ili kujua ukweli wa habari iliyochapishwa katika toleo na. 400 la Julai 18-20 yenye kichwa cha habari “ Warembo TZ wapiga picha za x tupu? Anadai kinachomsikitisha siyo kama habari hiyo ni ya kweli au ya kubuni bali ni picha zilizotumika.

Chahali anaamini kuwa anajua kila kitu! Jambo ambalo siyo kweli na haliwezekani.

Hata hivyo, nataka nimfahamishe kuwa habari inayoandikwa na mwandishi anayejifanya kuwa na taaluma zote kichwani ina madhara makubwa kwa jamii kwa sababu huweza kumuumiza mtu ama kumsababishia kifo.

Hivi Chahali alitaka tuambatanishe na mtandao wanaopatikana warembo hao ili athibitishe kuwa ni watanzania? Haoni kuwa kwa kufanya hivyo ni ‘kuwapromoti’ mabinti hao? Kama kulikuwa na ulazima kwanini yeye hakuweka bayana mtandao aliodai kuwa alitumiwa na rafiki yake uliokuwa ukikanusha habari yetu?

Nawaheshimu sana watanzania na siwezi kamwe kuwafanya wajinga kwa kuwapa habari “sensational” ambazo hazina ukweli! Nataka kuwathibitishia watanzania wote kuwa RISASI ni gazeti linalozingatia kanuni na maadili ya uandishi wa habari.

Baada ya kusema hayo, naomba niweke wazi ‘link’ za mtandao ambao kila mwenye nafasi aweze kuupitia ili kuona nani ni muongo kati ya Chahali na Gazeti la Risasi. Mtandao huo ni http://swallowmyjuice.hi5.com ambapo wote wanadai ni wakazi wa Dar es Salaam, Tanzania sasa Risasi limedanganya nini?

Kimsingi simkatazi Chahali siku nyingine kuandika maoni yake, kwani maoni ni miongoni mwa njia za kupata ukweli, lakini mara unapoupata unapaswa kuhakikisha unaufuata!

Kama Chahali alikuwa hajui basi nichukue nafasi hii kumfahamisha kwa ufupi kuwa, kuna baadhi ya mambo ambayo hufanya habari kuwa habari ‘elements that make news to be newsworthiness’ ambazo ni kama zifuatazo.

Kwanza kabisa kuna (proximity) ukaribu wa habari husika na jamii lengwa, (prominence) inamhusu mtu gani maarufu, (impact) madhara ama umuhimu wake kwa jamii, (conflict) mkingamo wa mawazo, (timeliness) limetokea lini, (novelity) je tukio hilo ni la kawaida ama si la kawaida na (human interest) uvutaji wa hisia za watu.

Kutokana na sifa hizo ni ukweli ulio wazi kuwa wahariri wa gazeti la RISASI tulikuwa na kila sababu ya kutoa habari ile kwani tukio lenyewe si la kawaida katika jamii yetu labda Chahali anaona ni jambo lisilowezekana kutokea nchini kwetu na kusahau kuwa tukio hilo ni moja ya athari za utandawazi.

Sitaki kutumia muda mwingi kuelezea sifa zote zilizosababisha kuchapisha habari hiyo ila kimsingi Chahali ni miongoni mwa watu wanaosemwa na mwanafalsafa wa siku nyingi, Permanides kuwa kuna watu wanachanganya kati ya ukweli kadiri unavyojitokeza kwao na ukweli halisi na kusisitiza kuwa ni vizuri kuangalia kitu kama kilivyo na si vinginevyo.

Tanzania ni nchi yetu na tuna jukumu kubwa sana mbele yetu katika dunia hii tuliyopo ya ‘information age’ ambalo ni kuhakikisha tunaandika habari za uhakika ili kuiwezesha jamii yetu kupata maisha bora! Sasa kaka Chahali, vya mung’unya, unatafuna, inakuwaje?

Kuna kila sababu ya uongozi wa gazeti hili kuamini kuwa Chahali aliamua kutuchafua ili aweze kupata umaarufu kwani alijua kuwa akifanya hivyo ataandikwa sana na magazeti hivyo, kuanzia hapo atajulikana kwani tangu mwaka 2006 hadi sasa ana watu 2000 tu waliotembelea blog yake, wakati watanzania wengine hupata watu zaidi ya 500 kwa siku.

Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa namba +255 0715 888887. mwakilaga.blogspot.com

DENTI AFUMWA 'AKIKANDAMIZWA KIBARA' USIKU WA MNANE


Catherine Kassally na Mariam Mndeme waliokuwa Morogoro

Mwanafunzi wa darasa la tano wa shule moja ya Msingi, mkoani
Morogoro aliyefahamika kwa jina moja la Emmy, amefumwa akiwa na

jamaa mmoja ‘mtu mzima’ wakiponda raha na mambo mengine machafu.
Denti huyo alifumwa na waandishi wetu, saa nane usiku, Jumatano
wiki hii kwenye sherehe za wakulima Nane Nane, katika viwanja
vya Mwalimu Nyerere, mjini Morogoro.

Denti huyo akiwa anaonekana ‘kuunyaka mtindi’ alikuwa
amekubatiwa na jamaa huyo ambaye jina lake halikuweza
kupatikana mara moja mbele ya kadamnasi ya watu katika grosari
moja iliyomo uwanjani humo.

Binti huyo ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 12 na 14,
ambaye haikufahamika shule aliyokuwa akisoma, alikuwa amepakatwa
na jamaa huyo huku wakibusiana.

Waandishi wetu pamoja na baadhi ya watu waliokwenda katika
viwanja hivyo, waliwashuhudia binti huyo na jamaa yake
anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 35-40 jambo
lililowafanya wawashangae na kulaani kitendo hicho kichafu.

Hata hivyo, baada ya vitendo hivyo kuendelea kukithiri baadhi ya
watu waliokuwepo katika eneo hilo walianza kuwakemea kwa
kuwataka waondoke, vinginevyo wangewaitia polisi.

Licha ya tishio hilo, wawili hao waliendelea kufanya uchafu wao
huku wakidai kuwa wasingewafanya chochote kwani walikuwa katika
raha zao.

Hata hivyo, jamaa aliyekuwa na denti huyo naye alianza kufoka
akidai kuwa wanawaonea kwavile ni waswahili kwani wangekuwa
wazungu wagewaacha.

‘’Hata kama mtawaita polisi, hawawezi kutufanya kitu kwani nyie
ndio mnaotutazama, kama mnaona noma basi msituangalie,
wangefanya wazungu mngesemasema maneno hayo?,” Alihoji jamaa
huyo.

Aidha, watu hao walishangaa wakidai kuwa jamaa huyo ni kubwa
kiumri hivyo alikuwa akimuonea kwa kumrubuni binti huyo
kutokana na umri wake kuwa mdogo.
Hata hivyo, katika hali ya kushangaza binti naye alianza kutoa

maneno ya kuwashambulia watu hao na kudai kuwa wawaache kwani
jamaa aliyekuwa naye anammudu licha ya kuonekana mkubwa kuliko
yeye.

“Mwacheni mpenzi wangu mwenyewe ninammudu na wala si mkubwa
kwangu mimi namuona kama mtoto mwenzangu,” alisema denti huyo.
Baada ya kuona wapenzi hao wanaendelea kufanya uchafu huo,
waandishi wetu walipowapiga picha ambapo awali waliduwaa lakini
baadaye walishtuka na kuacha.

Waandishi wetu pamoja na watu wengine waliokuwepo hapo
walipowasogelea, jamaa alinyanyuka na kumwacha binti huyo
ambaye aliomba msamaha baada ya kuambiwa kuwa picha yake
ingechapishwa kwenye gazeti.

“Mnisamehe dada zangu, haya ni maisha yangu na ni siri yangu,
shuleni kwangu hawajui, wala nyumbani kwetu hawafahamu sasa
mkitoa picha hiyo nitapigwa hadi kuuawa, niko tayari kuwapeni
hata fedha” alisema msichana huyo huku akimwaga chozi.
Msichana huyo aliondoka baada ya kuona kuwa ombi lake
halisikilizwi na wanahabari hao.

Tumelazimika kuziba sura ya binti huyo kutokana na sababu za
kimaadili - Mhariri.

Friday, August 10, 2007

THOMAS MLAMBO WA SUPER SPORT ATUA BONGO!

Jamaa ni miongoni mwa watu wanao 'uza sura' sana barani Afrika na baadhi ya nchi za Ulaya,hasa kwa wale wapenzi wa michezo na watazamaji wa chaneli pekee ya mpira barani afrika 'SUPER SPORT', huyu si mwingine bali ni THOMAS MLAMBO! Katua Bongo kwa ziara fupi ya kikazi,hapa akifanya press conference katika hoteli ya Holiday, jijini Dar,Ijumaa mchana.
Thomas Mlambo akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano namedia. Uwanja Mpya utakapoanza kutumika, jamaa wa Super Sport watakuwa wakirusha mpira LIVE!

Lucy Kiwhele (kushoto) naFuraha Samalu, viunganishi vikubwa vya media na MultiChoice Tanzania


Angela Msangi (kushoto) mwandishi wa TVT akihojiana na Meneja Uhusiano wa MultiChoice TZ, Lucy Kiwhele, katika Hoteli ya Holiday Inn, mapema Ijumaa



Mazagazaga ya kula ya Holiday Inn




Mhariri wa gazeti la michezo, Sport Starehe, Masoud Sanani (kushoto) akipozi Thom





Thomas Mlambo (kulia)akiwana 'mdau' wa blog hii,Mrisho